Baada ya kupoteza kazi yangu, niliamini kwamba ningepata nyingine ndani ya muda mfupi.

Nilikuwa na uzoefu wa kazi, nilikuwa tayari kufanya kazi kwa bidii, na nilikuwa na matumaini kwamba waajiri wangetambua uwezo wangu. Lakini mambo hayakwenda kama nilivyokuwa nimepanga. Miezi ilianza kupita.

Nilituma maombi ya kazi sehemu nyingi. Kila nilipoona tangazo la kazi, nilihakikisha nimetuma maombi yangu kwa wakati. Mara nyingine niliitwa kwenye usaili, lakini sikuwa nikichaguliwa. Mwaka mmoja ulipita. Kisha mwaka wa pili ukafika.

Kwa kweli hali ile ilianza kuniumiza sana. Niliona marafiki na watu niliokuwa nao wakipiga hatua maishani huku mimi nikiendelea kukaa nyumbani nikisubiri simu ambayo haikufika.

Kilichoniumiza zaidi ni kwamba nilianza kujiuliza kama tatizo lilikuwa mimi.

Baada ya kufeli usaili mara nyingi, confidence yangu ilishuka. Kila nilipoitwa kwenye interview mpya, nilikuwa naingia nikiwa tayari nimejiambia kwamba sitapata kazi. Kadri muda ulivyopita, matumaini yangu yalizidi kupungua.

Kulikuwa na siku nilizotaka kuacha kutuma maombi kabisa. SOMA ZAIDI.
Share To:

Post A Comment: