Miaka miwili iliyopita, nilikuwa nikifanya biashara yangu kwa matumaini makubwa.

Biashara ilikuwa inaendelea vizuri na nilikuwa nimejijengea wateja wengi wa kudumu. Kwa sababu ya uaminifu tuliokuwa nao, mara nyingine nilikuwa nikiwaruhusu baadhi yao kuchukua bidhaa kwa mkopo na kulipa baadaye.

Mmoja wao alikuwa mteja niliyemwamini sana.
Tulikuwa tumefanya biashara kwa muda mrefu bila matatizo yoyote. Ndiyo maana sikuona shida aliponiomba bidhaa zenye thamani kubwa kwa ahadi kwamba angelipa ndani ya muda mfupi.

Lakini mambo hayakwenda kama nilivyotarajia.
Siku za malipo zilipofika, simu zake zilianza kutopatikana. Ujumbe wangu haukujibiwa.

Nilijaribu kumtafuta kupitia marafiki na watu waliomfahamu, lakini sikufanikiwa. Kwa kweli nilihuzunika sana. 

Kiasi cha fedha alichokuwa anadaiwa kilikuwa kikubwa kwa biashara yangu. Hasara ile ilinifanya nipunguze baadhi ya mipango yangu na hata kushindwa kufanya manunuzi muhimu ya biashara kwa wakati.

Kadri miezi ilivyopita, matumaini yangu yalizidi kupungua. SOMA ZAIDI.

Share To:

Post A Comment: