Mkuu wa Chuo cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Prof. Haruni Mapesa amewataka Wafanyakazi wa MNMA kuendelea kufanya kazi kwa furaha, Uadilif na kuweka maslahi ya Taasisi mbele kwa kuhakikisha huduma bora zinatolewa kwa Wanafunzi na Watumishi kwa moyo na kufanya hivyo ni utumishi kama ilivyo utumishi wa Mungu, kwani kila kazi unayoifanya kwa ajili ya watu basi hiyo ni kazi ya Mungu.

Prof.Mapesa ameyasema hayo leo wakati wa kuwapongeza Watumishi hodari katika uwajibikaji wa utumishi wa umma kwa mwaka 2025/2026 kwa wale wote waliopata fursa ya kuwa Wafanyakazi bora, na kusisisitiza kuwa Watumishi waendelee kufanya kazi kwa kuzingatia Misingi ya utumishi wa umma na huo ndiyo uwe utamaduni wa kila siku.

Kwa upande wake Naibu Mkuu wa Chuo anaesimamia Taaluma, Utafiti na Ushauri wa Kitaaluma Prof. Richard Kangalawe amesema Ushindi ni heshima huku akiwataka watumishi wengine kuendeela kuwajibika katika nafasi zao kwa lengo la kutimiza malengo ya Taasisi.



Naye Naibu Mkuu wa Chuo anaesimamia Mipango, Fedha na Utawala Prof.Evaristo Haulle alisema mchakato wa kupata Mfanyakazi bora ulikuwa ni wa huru na haki ambapo vigezo mbalimbali vilizingatiwa ikiwemo Nidhamu ya mtumishi , Utendaji kazi wa mtumishi,(PEPMIS) na Mienendo mbalimbali, hivyo dosari zote zilizojitokeza zilishughulikiwa ipasavyo.

Nao viongozi wa Vyama vya Wafanyakazi Debora Donati wa THTU na kwa upande wa  RAAWU  Hashimu Mtongola  kwa pamoja wameipongeza Menejimenti kwa hafla hiyo fupi ambayo inatoa motisha na kuongeza morali ya kazi kwa Wafanyakazi na pia wameomba uongozi ufikirie kujumuisha Wafanyakazi wote kwa hafla ya namna hiyo wakati mwingine.



Wafanyakazi bora wa Taasisi kwa mwaka huu Filbert Nyakasi upande wa Wanataaluma  na Amedeus Mchau upande wa Waendeshaji wameshukuru uongozi kwa kutambua jitihada zao na mchango wao katika kutimiza majukumu ya kila siku na wameahidi kuendelea kufanya kazi kwa Uadilifu, Nidhamu kwa  kushirikiana na Wafanyakazi wengine.


Wafanyakazi wote hodari wamentunukiwa vyeti vya kutambuliwa na zawadi ya fedha, ambapo zoezi limejumuisha Wafanyakazi wote bora wa Kampasi ya Kivukoni, Karume na Pemba.


Imetolewa na:

Kitengo cha Mawasiliano na Masoko

ChUO CHA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE

25.05.2026

Share To:

Post A Comment: