Wajumbe wa Bodi ya Chuo cha Maji (Water Institute) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi hiyo Dr. Maulid J. Maulid wamekutana Aprili 28, 2026 jijini Dar Es Salaam kwa kikao cha 46 cha Bodi hiyo kujadili masuala ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utoaji wa huduma za kitaaluma na miradi ya maendeleo itakayoboresha ufundishaji na ujifunzaji.
Bodi ya Chuo inaundwa na wajumbe saba ambao ni Dr. Felician Komu, CPA Lucy Mrikaria, Dr. Maulid J. Maulid (Mwenyekiti), Professor Adam Karia (Katibu/Mkuu wa Chuo cha Maji), Professor Said Ally, Ms. Jane Gonsalves na Engineer Charles Mafie (Mkurugenzi wa Usambazaji Wizara ya Maji).














Post A Comment: