Wananchi wameamua kujitoa kwa hali na mali kuhakikisha wanamlinda, kumtetea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa gharama yeyote Ile.
Hayo yamejidhirisha kwenye uzinduzi wa ofisi ya kwanza na ya kihistoria nchini ya TK Movement uliotokana na nguvu za Wananchi ambapo uzinduzi huo wa ofisi umefanywa na Afisa Tarafa Lisekese Emmanuel Shilatu kwenye Kijiji cha Miwale kilichopo Kata ya Msikisi.
Akizungumza na Wananchi wa Kata ya Msikisi, Shilatu aliwasihi Wananchi kuongeza Utaifa, Uzalendo kwa Taifa lao la Tanzania kwa kujivunia Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kujivunia Serikali yao, kujivunia na kuyasema maendeleo yaliyopatikana nchini.
"Nawapongeza Wananchi wote kuhakikisha upatikanaji wa ofisi ya kwanza ya TK Movement. Ndugu zangu, akitokea Mtu akikwambia Tanzania tuna nini mwambie tuna amani, tuna maendeleo na tuna Rais Samia Mzalendo, Mchapa kazi, hodari, mtekelezaji na mfuatiliaji. Akikuuliza maendeleo yapi mpeleke muonyeshe miradi ya maendeleo ambayo ipo Kila sehemu kwenye sekta za afya, elimu, maji, miundombinu nk. Waonyesheni pembejeo za kilimo mnazopewa bure na Rais Samia. Hakikisheni mnawaeleza Watu utekelezaji wa ilani ya uchaguzi CCM unaofanywa na Serikali" Alisema Shilatu.
"Tunapoelekea kwenye uchaguzi Mkuu huu wa kuwachagua Madiwani, Wabunge na Rais hakikisheni mnadumisha amani na utulivu lakini pia mjiepushe na vitendo vya rushwa." Alisisitiza Gavana Shilatu.
Nae Mwananchi aliyejitambulisha kwa jina la Rauphu Said amesema Wananchi wanajivunia Serikali yao napo tayari kuitetea na kumtetea Mhe. Rais Samia.
"Mimi kama kijana na Vijana wenzangu tunayaona maendeleo yanayoendelea kupatikana na kukua nchini yanayotupelekea kuamua kuitetea Serikali iliyopo Madarakani na kumlinda Rais Samia kwa wivu mkubwa." Alisema Rauphu.
TK Movement ni mtandao unaofanya kazi ya kuhamasisha Vijana na Wanawake katika ushiriki wao wa shughuli za maendeleo nchini ili kuchochea Kasi ya maendeleo katika Taifa letu.
Post A Comment: