WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dk. Selemani Jafo,akizungumza wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Kudhibiti Bidhaa Bandia Duniani, yaliyoandaliwa na Tume ya Ushindani (FCC),yaliyofanyika leo Juni 25,2025 jijini Dodoma.

......

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dk. Selemani Jafo,amewataka wafanyabiashara wote wanaozalisha bidhaa nchini pamoja na waagizaji kutoka nje kuhakikisha wanazingatia sheria ya alama za bidhaa, ili kudhibiti uingizaji, usambazaji na uuzaji wa bidhaa bandia katika soko la Tanzania Bara.

Dkt. Jafo ameyasema hayo leo Juni 25,2025 jijini Dodoma kwenye maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Kudhibiti Bidhaa Bandia Duniani, yaliyoandaliwa na Tume ya Ushindani (FCC).

Dkt. Jafo amesema kuwa bidhaa bandia si tu zinahujumu uchumi wa nchi, bali pia huhatarisha afya na usalama wa wananchi, kupoteza mapato ya serikali, na kukatisha tamaa wabunifu halali wa bidhaa.
“Wafanyabiashara wote wanapaswa kuelewa kuwa Sheria ya Alama za Bidhaa inapiga marufuku kuingiza, kutengeneza, kuuza au hata kuhifadhi bidhaa bandia. Adhabu yake ni kali, ikiwemo kifungo na faini,” amesema Dkt. Jafo.
Aidha, ameiagiza Tume ya Ushindani (FCC) kushirikiana na wamiliki wa nembo na vyombo vya uwakilishi wa wafanyabiashara ili kutoa elimu ya kutosha kuhusu sheria hiyo na madhara ya bidhaa bandia.
“Ushirikiano kati ya FCC na taasisi za kitaifa na kimataifa ni muhimu kwa kuboresha mbinu za udhibiti, ikiwemo matumizi ya teknolojia ya kisasa kutambua bidhaa bandia sokoni,” amesema Dkt Jafo
Dkt.Jafo amesema kuwa udhibiti wa bidhaa bandia si jukumu la serikali peke yake, bali ni wajibu wa kila mdau katika mnyororo wa biashara.

Hata hivyo Dkt.Jafo,amesisitiza umuhimu wa matumizi ya teknolojia ya kisasa kutambua bidhaa bandia kama matairi ya magari, vyakula, nondo na nguo.

“Bidhaa kama nondo zisipozingatia viwango zinaweza kusababisha majanga kama kuporomoka kwa majengo. Hii si tu tishio kwa maisha ya watu bali ni pigo kwa uchumi wetu. Tunahitaji kulinda ubora wa bidhaa na kusimamia sheria ipasavyo,” amesema Dkt.Jafo

Naye, Mwakilishi wa Kamati ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, Pauline Gekul,ametoa wito kwa Serikali kuongeza jitihada za udhibiti wa bidhaa bandia, hasa kwenye sekta za simu na vyakula.

“Wananchi wa chini bado hawana elimu ya kutambua bidhaa bandia. Ni muhimu elimu ikatolewa zaidi, na wadhibiti wajitambulisha kwa jamii ili kujenga uelewa wa viwango vya bidhaa nchini,” alisema Gekul.

Kadhalika, Mwenyekiti wa Bodi ya FCC, Dk. Aggrey Mlimuka, amesema kuwa lengo la udhibiti wa bidhaa bandia ni kuendeleza mazingira ya biashara na kulinda maslahi ya walaji.

Dkt.Mlimuka amefafnua kuwa FCC inashirikiana na wadau wa Zanzibar kuelimisha kuhusu madhara ya bidhaa bandia, kufanya ukaguzi, na kuchukua hatua dhidi ya wahusika.

Awali, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Khadija Ngasongwa, amesema kuwa ofisi zao za kanda zinazohudumia zaidi ya mikoa 16 zimeendelea kutoa elimu kwa wafanyabiashara na kufanya ukaguzi ili kubaini bidhaa zisizo halali.

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dk. Selemani Jafo,akizungumza wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Kudhibiti Bidhaa Bandia Duniani, yaliyoandaliwa na Tume ya Ushindani (FCC),yaliyofanyika leo Juni 25,2025 jijini Dodoma.

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dk. Selemani Jafo,akizungumza wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Kudhibiti Bidhaa Bandia Duniani, yaliyoandaliwa na Tume ya Ushindani (FCC),yaliyofanyika leo Juni 25,2025 jijini Dodoma.

KAIMU Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Khadija Ngasongwa, akizungumza wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Kudhibiti Bidhaa Bandia Duniani, yaliyoandaliwa na Tume ya Ushindani (FCC),yaliyofanyika leo Juni 25,2025 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Selemani Jafo (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Kudhibiti Bidhaa Bandia Duniani, yaliyoandaliwa na Tume ya Ushindani (FCC),yaliyofanyika leo Juni 25,2025 jijini Dodoma.

SEHEMU ya washiriki wakimsikiliza Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Selemani Jafo (hayupo pichani) wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya Siku ya Kudhibiti Bidhaa Bandia Duniani, yaliyoandaliwa na Tume ya Ushindani (FCC),yaliyofanyika leo Juni 25,2025 jijini Dodoma.

Halmashauri Kuu ya Utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kilombero Mkoani Morogoro imeipongeza Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika Vijijini vyote 110 vya Wilaya hiyo pamoja na Vitongoji 283 kati ya 458.

Pongezi hizo zimetolewa leo na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kilombero, Mohamed Msuya wakati wa uwasilishwaji wa taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020-2025 huku akiwapongeza Madiwani, Wabunge na Watendaji wa Serikali.

“Tuwapongeze sana Waheshimiwa Madiwani, Wabunge kwa kusimamia Ilani ya CCM katika Wilaya yetu kufanikiwa. Lakini pia tuwapongeze sana Watendaji wa Serikali kwa kusimamia maelekezo ya ilani,” amepongeza Mwenyekiti huyo.

Awali akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa Ilani ya CCM kwa Wajumbe wa Mkutano huo, Mkuu wa Wilaya ya Kilombero, Mhe. Dunstan Kyobya amempongeza na kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha zilizowezesha kutekelezwa kwa miradi iliyoahidiwa katika Ilani ya CCM katika Wilaya hiyo.

Kwa upande wake, Meneja wa Miradi kutoka REA, Mhandisi Romanus Lwena ameahidi kuwa Wakala utaendelea kufanya kazi usiku na mchana kuhakikisha vitongoji ambavyo bado havijafikiwa na umeme vinapata umeme ili lengo la Serikali la kuendelea kuboresha maisha ya Watanzania linatimia.

Hayo yamesemwa leo tarehe 25 Juni, 2025 na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu – ADEM Dkt. Maulid J. Maulid alipokuwa akifungua rasmi mafunzo ya Utawala Bora wa Elimu kwenye Mamlaka za Serikali za Mitaa yanayotolewa na ADEM kwa Maafisa Elimu Kata 352 kutoka Mkoa wa Dodoma na Kilimanjaro.

Mafunzo hayo yamelenga kuwawezesha Maafisa Elimu Kata kusimamia kwa ufanisi shughuli zote za elimu katika ngazi ya Kata.

Dkt. Maulid J. Maulid amesema Maafisa Elimu Kata wana wajibu wa kutambua na kutafsiri kwa vitendo maono ya Serikali kwa kuhakikisha wanakuwa wasimamizi wa kwanza wa maboresho makubwa yaliyofanyika katika sekta ya elimu kwa kuboresha Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014 Toleo la 2023 na Mtaala ulioboreshwa ili kufikia lengo la Serikali la kuboresha na kuimarisha sekta ya elimu nchini.

“Mabadiliko na mageuzi yanayotegemewa kutokea kwa utekelezaji wa Sera ya Elimu na Mtaala ulioboreshwa yako kwenye meza zenu kama wasimamizi wa kwanza wa shughuli za elimu katika ngazi ya Kata. Tunawaomba mwende mkasimamie ipasavyo mageuzi hayo na tuone matokeo kuanzia kwenye ngazi ya Shule na Kata kwa kwenda kutekeleza kwa vitendo yale mtakayojifunza kwenye mafuzo haya kwani hayo ndio yatakuwa dira ya kuwasaidia kufanya usimamizi fanisi wa shughuli zote za elimu katika ngazi ya Kata na hatimaye lengo la Serikali kufikiwa”. Amesema Dkt. Maulid.

Aidha, Dkt. Maulid amesisitiza Maafisa Elimu Kata hao kuitambua, kusoma, kuelewa na kutekeleza miongozo yote inayotolewa na Mamlaka zinazosimamia elimu nchini ikiwa ni pamoja na Ofisi ya Kamishna wa elimu ili iwasaidie katika utekelezaji wa majukumu yao ya usimamizi wa shughuli za elimu kwenye ngazi ya Kata kwa ufanisi.

Vilevile Dkt. Maulid amesisitiza usimamizi wa nidhamu, uwajibikaji, ufundishaji na ujifunzaji mahiri wenye kuinua ubora wa elimu inayotolewa shuleni.

Nae Makamu Mkuu wa Chuo Taaluma Dkt. Alphonce J. Amuli amesema washiriki wa mafunzo hayo watajengewa uwezo katika maeneo ya Uongozi, Usimamizi na Utawala katika Elimu, Utawala Bora katika Elimu, Uandaaji wa Mpango wa Jumla wa Maendeleo ya Elimu Ngazi ya Serikali za Mitaa, Ufuatiliaji na Usimamizi Fanisi wa Shule, Usimamizi wa Ujenzi wa Miundombinu ya Shule, Ukaguzi wa Ndani, na Ushirikishwaji wa Jamii na Utatuzi wa Malalamiko katika Elimu. Dkt. Amuli pia amesema kuwa ni dhahiri kwamba, maeneo hayo yatakayowezeshwa yatasaidia kuimarisha usimamizi na uendeshaji wa shule kwa ufanisi.

Mafunzo ya Utawala Bora wa Elimu katika Mamlaka za Serikali za Mitaa yanafanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 25 – 27 Juni, 2025 ADEM Bagamoyo na yamefadhiliwa na mradi wa BOOST chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 






 


Na. Saidina Msangi, WF, Dodoma.

Serikali imesema kuwa Tanzania haitapata athari za moja kwa moja kutokana na mafanikio au changamoto zozote katika Umoja wa BRICS (Brazil, Russia, India, China na Afrika Kusini), zinazoweza kutokea katika sekta ya kiuchumi na fedha hususani ya kujiondoa kwenye Dolarisation kwa kuwa sio nchi mwanachama wa BRICS.

Hayo yalisemwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mheshimiwa Zahor Mohammed Haji (Mwera), aliyeuliza faida na hasara ya Tanzania kutokana na msimamo wa nchi za BRICS ambazo zimejipanga kujiondoa kwenye mfumo wa Dolarisation.

Alisema Serikali ya Tanzania imekuwa na ushirikiano wa muda mrefu na nchi za BRICS (Brazil, Russia, India, China na Afrika Kusini) katika nyanja mbalimbali ikijumuisha masuala ya kiuchumi, biashara na diplomasia kwa kuendelea kuwepo kwa balozi za nchi hizo hapa nchini na Tanzania kuwa na balozi katika nchi hizo.

’’Kwa sasa Tanzania sio mwanachama wa BRICS ila inashiriki katika mikutano ya BRICS kama observer, hivyo mafanikio au changamoto zozote katika umoja huo zinazoweza kutokea katika sekta ya kiuchumi na fedha hususani ya kujiondoa kwenye Dolarisation, hatutakuwa na athari za moja kwa moja kwa kuwa sio wanachama wa BRICS,’’ alifafanua Mhe. Chande.

Mhe. Chande alisema mahusiano ya Tanzania na nchi hizo yanadumishwa kwa kuendelea kuwepo kwa balozi za nchi hizo hapa nchini na Tanzania kuwa na balozi katika nchi hizo.

Aliongeza kuwa mahusiano hayo yanaendelea kuleta mafanikio chanya kwa Serikali ya Tanzania kwa kutumia fursa za kiuchumi zinazopatikana katika nchi hizo ambazo pia zinaimarisha mahusiano ya uwili baina yake (bilateral engagement).

.


Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) imepongeza utendaji bora wa Shamba la Miti la West Kilimanjaro, huku ikielezea kuridhishwa na namna linavyoboresha maisha ya wananchi na kuchangia maendeleo ya Taifa kupitia uzalishaji endelevu wa mazao ya misitu.

Akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Meja Jenerali Dkt. Mbaraka Mkeremy, wakati wa ziara ya kikazi iliyofanyika Juni 24, 2025, Mjumbe wa Bodi Dkt. Siima Bakengesa alisema kuwa Shamba hilo limeonyesha mfano wa kuigwa katika kuendeleza rasilimali za Taifa kwa manufaa ya wananchi na kizazi kijacho.

"Tumefurahishwa na kazi nzuri inayofanyika hapa West Kilimanjaro. Tumeona namna shamba hili linavyochangia pato la Taifa kupitia uzalishaji wa miti na pia kuwanufaisha wananchi kwa kuwashirikisha katika shughuli mbalimbali za kiuchumi kama kilimo na ufugaji wa nyuki,” alisema Dkt. Bakengesa.

Dkt. Bakengesa alisifu uwekezaji unaoendelea kufanyika katika kuboresha mazingira ya kazi kwa watumishi, ikiwemo ujenzi wa nyumba za makazi, ukarabati wa majengo na uboreshaji wa miundombinu ya msingi.

"Tunapongeza juhudi za TFS katika kuboresha mazingira ya kazi kwa watumishi. Haya ni mambo muhimu yanayochochea ufanisi na kuongeza motisha kazini,” aliongeza.

Kwa upande wake, Mhifadhi Mkuu wa Shamba hilo, Bw. Robert Faida, alieleza kuwa shamba hilo limeendelea kutekeleza miradi ya kimkakati ya uwekezaji kwa kushirikiana kwa karibu na makao makuu ya TFS.

"Katika miaka ya hivi karibuni, tumeimarisha huduma mbalimbali ikiwa ni pamoja na miundombinu ya makazi, vitendea kazi, na ushirikiano na jamii. Tunaendelea kuboresha zaidi kwa kadri rasilimali zinavyoruhusu,” alisema.

Akizungumzia nafasi ya sekta binafsi katika kuendeleza misitu, Bw. Faida alihimiza wawekezaji kuanzisha viwanda vya kisasa vya kuchakata mazao ya misitu, huku akieleza kuwa mahitaji ya mbao nchini yanaendelea kuongezeka na kutoa fursa pana kwa uwekezaji.








Chuo cha Uhasibu Arusha pamoja na Chuo cha  Heriot-Watt University (UK) kupitia shule ya Biashara wamesaini makubaliano kuhusu tafiti.

Akizungumza katika utiaji saini wa makubaliano hayo, Mkuu wa Chuo Profesa, Eliamani Sedoyeka alieleza  kuwa Chuo Kikuu cha Heriot Watt ni moja ya taasisi za juu zinazoheshimika duniani na ushirikiano huo ni muendelezo wa IAA kujitanua kimataifa ambayo pia ni ajenda ya serikali ya awamu ya sita.

Prof. Sedoyeka ametaja maeneo makubwa ya ushirikiano kuwa ni katika uendeshaji wa programu za pamoja, tafiti na kubadilishana uzoefu kati ya wahadhiri na wanafunzi. Haya yote ni kwa ajili ya kuboresha uzoefu wa kujifunza na kufundisha na sio tu kwa IAA bali pia kwa Heriot-Watt.

Naye  Profesa ,Angus Laing ambaye ni Mkuu wa Kitivo cha Edinburgh Business School amesema chuo chao kimefurahi kuingia makubaliano na IAA na wanaamini ushirikiano  huu utakuwa na manufaa kwa pande mbili.

Ameongeza kuwa wakati wakitafuta Chuo cha kushirikiana nacho Tanzania, IAA ilikuwa Chuo kilichopendekezwa hata kupitia ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza na wamegundua tunahistoria na maadili ya msingi (values) yanayofanana.

Profesa Angus Laing ameeleza kwa sasa IAA imeingia rasmi kwenye mtandao wao wa Vituo vyao vya kimataifa ambapo wanavituo vitano vilivyoko Uingereza (UK), Dubai na Malaysia.

Naye Dk,Mwamini Tulli ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi la Chuo amepongeza taasis zote mbili na ameahidi kuwa Baraza la Uongozi linatoa ushirikiano katika kuhakikisha makubaliano hayo yanakuwa na kufanikiwa kwa manufaa ya taasisi husika lakini pia nchi zetu.












 Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Mhe. Dkt Stergomena Tax (Mb,) amefunga rasmi mafunzo ya mwaka mmoja ya Ukamanda na Unadhimu, katika Mahafali ya 39 ya Chuo cha Ukamanda na Unadhimu Tanzania yaliyofanyika katika Viwanja vya chuo hicho, Duluti Arusha


Mahafali hayo ambayo Waziri wa Ulinzi na JKT alikuwa mgeni rasmi yalihusisha jumla ya Maafisa wahitimu 71 toka Jeshi la Wananchi la Tanzania na Maafisa wahitimu toka nchi marafiki.

Katika Mahafali hayo wahitimu hao pia wa kozi ya Ukamanda na Unadhimu pia walitunukiwa Shahada za Umahiri na stashahada ya Masuala ya Ulinzi na Usalama, mafunzo ambayo yaliendeshwa sambamba na kozi ya ukamanda na unadhimu.

Katika mahafali hayo, Waziri wa Ulinzi alisema amefurahishwa kupewa nafasi ya kuongoza Sherehe za Mahafali ya 39 ya Ukamanda na Unadhimu chuoni- Duluti na akatoa pongezi kwa Maafisa wote Wanafunzi 71 waliohitimu mafunzo hayo.

Waziri Stergomena Tax akawapongeza kwa bidii, ustahimili wa mafunzo makali na kuonyesha nidhamu, ujasiri, uthabiti na kujitolea unaohitajika ili kupata kumaliza kozi hiyo mashuhuri ya kimataifa. Na akawaambia wahitimu hao wanapaswa kujivunia sana mafanikio hayo.

Kwa Upande wa Maafisa Wahitimu wanawake, Waziri wa Ulinzi amewapongeza na kuwaambia wahitimu hao kuwa, wanawake ni sehemu muhimu ya jumuiya ya kijeshi, Uwepo wao katika kozi ya 39 ya ukamanda na unadhimu ni ushuhuda hai kwamba wanajeshi wetu wameunganishwa zaidi kulingana na jinsia kuliko hapo awali.

Waziri Tax akaongeza kwa kuwaambia wahitimu hao wanawake kwamba, kuhitimu mafunzo hayo ni kielelezo tosha cha kuonyesha kuwa wanawake wanaweza kutimiza majukumu yao katika kada sekta ya Ulinzi na Usalama kwa ufanisi na weredi bila kujali jinsia.

Amesema Tanzania kuongozwa na Rais wa Kwanza mwanamke Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ni hatua muhimu kwa wanawake katika uongozi wa juu, na kama Amiri Jeshi Mkuu, Uongozi wake bora unatuma ujumbe mzito kuhusu uwezo wa uongozi wa wanawake, na umuhimu wa kuwapa fursa sawa ili kuchangia amani, usalama na ustawi wa mataifa.

Aidha, Waziri Tax amewaambia wahitimu hao wa kozi ya Ukamanda na Unadhimu, “natambua mmepewa dhamana kubwa ya uongozi, mawazo ya kimkakati, na ustadi wa kufanya maamuzi, na mpo tayari kukabiliana na changamoto ambazo ziko mbele yenu.

Nyinyi ni viongozi wa baadaye wa Majeshi yetu ya Ulinzi, walinzi wa usalama wa Mataifa yetu, na walinzi wa uhuru wetu unaothaminiwa.

Waziri wa Ulinzi na JKT akawaambia wahitimu kuwa kama viongozi wajao watakabidhiwa majukumu ya kufanya maamuzi muhimu ya ulinzi na usalama wa mataifa yao akawaambia ana uhakika kwamba Elimu na ujuzi walioupata umewatayarisha, na utatumika kama msingi wa utekelezaji wa majukumu yao na kukabiliana na changamoto mbalimbali.

Waziri Tax akawakumbusha Maafisa wahitimu hao kwamba uongozi hauhusu vyeo na nyadhifa, bali ni kuonyesha na kuongoza njia, kuwatia moyo wengine kwa uwezo wao kamili na kufanya kazi pamoja kufikia lengo linalotarajiwa. Kwa hivyo akawataka kudumisha maadili ya heshima, uadilifu, nidhamu katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Ulimwengu tunaoishi, unabadilika mara kwa mara na changamoto tunazokabiliana nazo zinazidi kuwa ngumu na zisizotabirika, akawahimiza wahitimu wa kozi hiyo adhimu kwamba wamepewa zana na uwezo unaohitajika ili kukabiliana na changamoto hizo zinazoendelea kwa ujasiri na uthabiti.

Vile vile Waziri wa Ulinzi akazishukuru nchi marafiki za Jamhuri ya Burundi, Jamhuri ya Botswana, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Jamhuri ya Kiarabu ya Misri, Jamhuri ya Shirikisho la Ethiopia, Jamhuri ya Kenya, Ufalme wa Eswatini, Jamhuri ya Malawi, Jamhuri ya Msumbiji. , Shirikisho la Jamhuri ya Nigeria, Jamhuri ya Rwanda, Jamhuri ya Uganda, Jamhuri ya Zambia na Jamhuri ya Zimbabwe, kwa urafiki na ushirikiano wao katika kutoa maafisa kushiriki katika kozi hii ya Ukamanda na Unadhimu.

Waziri Stergomena Tax akawaambia nchi marafiki kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inathamini uhusiano wa kirafiki uliopo na nchi zao na ana imani uhusiano wa muda mrefu utaimarishwa kwa ushirikiano unaoendelea, ikiwa ni pamoja na ushiriki katika kozi zinazotolewa na Chuo Duluti.

Mahafali ya 39 ya Chuo cha Ukamanda na Unadhimu Duluti yamehudhuriwa pia na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Luteni Jenerali Salum Haji Othman, Wakuu wa Kamandi za Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Wakuu wa Vyuo ya Ukamaanda na Unadhimu vya Afrika Mashariki, Wakuu wa Vyuo ya Kijeshi ya Jeshi la Wananchi la Tanzania, Waambata Jeshi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania, Maafisa wakuu Majenerali toka Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania na Makamanda vikosi vya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.