Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, ametembelea hospitali mpya ya Mtewele iliyopo katika eneo la Block X, Njombe Mjini, na kushuhudia uwekezaji mkubwa uliotekelezwa na Mzee Philemoni Mtewele.

Katika mazungumzo na Mzee Philemoni Mtewele, Mhe. Mtaka amempongeza kwa kuamua kuwekeza mradi mkubwa nyumbani Njombe, akibainisha kuwa kukamilika kwa hospitali hii kutawawezesha wananchi wa Mkoa wa Njombe na hata wale kutoka maeneo mengine kupata huduma bora za afya kwa urahisi. “Hii ni hatua muhimu inayoongeza upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi na inaonyesha jitihada za kweli za maendeleo,” alisema Mhe. Mtaka.

Kwa upande wake, Mzee Mtewele alimshukuru Mkuu wa Mkoa kwa kutembelea mradi wa ujenzi wa hospitali na kuonyesha ushirikiano katika kuhakikisha jitihada za kuboresha sekta ya afya zinathaminiwa na serikali pamoja na wananchi.

Hospitali ya Mtewele ni mradi mkubwa wa kimfumo unaoashiria maendeleo katika sekta ya afya, huku ikitoa matumaini makubwa kwa wananchi wa Njombe kupata huduma za matibabu za kisasa na kwa gharama nafuu.













Share To:

Post A Comment: