Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu kwa kushirikiana na UNDP, imezindua nyaraka tatu muhimu za usimamizi wa maafa katika Wilaya ya Sumbawanga, mkoani Rukwa.


✅ Nyaraka zilizozinduliwa:


Mpango wa Kujiandaa na kukabiliana na maafa ya Wilaya (D-EPRP)


Mkakati wa Kupunguza Vihatarishi vya Maafa (D-DRRS)


Ripoti ya Tathmini ya Vihatarishi, Uwezekano wa Kutokea na Uwezo wa kukbailian na maafa (RVCA)



📅 Uzinduzi umefanyika tarehe 23 Julai 2025 na kuhudhuriwa na viongozi wa serikali, wadau wa maendeleo na wananchi.


🎙️ Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga, Mhe. Nyakia Chirukile:


> "Hii ni hatua muhimu kujenga mfumo wa utayari dhidi ya majanga kama mafuriko."




🎙️ Brigedia Jenerali (Mstaafu) Hosea Ndagalla, Mkurugenzi wa Idara ya Maafa OWM:


> "Ni utekelezaji wa Sheria ya Usimamizi wa Maafa Na. 6 ya 2022."




🎙️ UNDP Tanzania kupitia Bw. Godfrey Mulisa:


> "Mpango huu ni sehemu ya kusaidia jamii kujenga upya maisha yao na kuwa imara zaidi."




💬 Wadau wa maendeleo wametoa pongezi na kuahidi kushiriki kikamilifu kutekeleza mpango huu.



---


🟢 #Maafa2025 #Sumbawanga #UtayariDhidiYaMajanga #UNDP #OWM

Share To:

OSCAR ASSENGA

Post A Comment: