Na Magesa Magesa,Arusha


ZAIDI ya wananchi 1800 kutoka katika mokoa 22 hapa nchini wamepata msaada wa kisheria katika kampeni ya msaada wa kisheria ya mama samia ijulikano kama Samia Legal Aid inayoendelea katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Mkurugenzi wa kampeni ya Samia Legal Aid, Ester Msambazi amesema jana alipokuwa akuzungumzia kampeni hiyo katika maonyesho yanayoendelea jijini Arusha kuelekea siku ya mwanamke duniani, wameshapokea migogoro 677.

Amesema kuwa pia wamepkea migogoro 677 kati yake 136 imefanikiwa kutatuliwa kwa wenye migogoro kusameheana na kupeana mikono huku baadhi ya migogoro iliyoko ngazi ya mahakama wahusika wameandikiwa hati za mahakama na kutakiwa kufika mahakamani.

“Tumefanikiwa kupokea migogoro 677 na kupatia ufumbuzi migogoro 136, ambapo waliofika tumewaandikia makubaliano na kuwashauri kufika mahakamani wale wanaopaswa kufika huko,”amesema Msambazi

Amesema tofauti na migogoro ambayo wamekuwa wakiipokea kutoka katika mikoa mingine nchini, migogoro mingi ya Arusha inatokana na watu kudaiana mali, huku mikoa mingine migogoro ya mirathi imeonekana kuwa kinara namba mbili baada ya migogoro ya ardhi.

 

“Arusha kumekuwepo na changamoto kubwa ya migogoro ya madai baada ya migogoro ya ardhi na wanaofikisha madai wengi ni wanaume, tofauti na mikoa mingine tuliyotembelea, hata hivyo tumefanikiwa kutatua migogoro mingi na tunaendelea kuitatua,”amesema.

 

Msambazi amesema migogoro iliyobaki inaendelea kufanyiwa kazi na jopo la wanasheria walioko katika kampeni hiyo na endapo wahusika hawajaridhika na majibu wanayopatiwa huruhusiwa kwenda katika taasisi zingine kutafuta haki zaidi.

 

“Sisi tumekuja hapa kutoa haki, hakuna hata mmoja ambaye tunafanya upendeleo lakini kuna baadhi ambao wao huwa hawataki kushindwa wala kupatanishwa wakiona hawawezi kupatana sisi tunawaruhusu kwenda mbele kutafuta haki zaidi,”amesema.

 






Share To:

Post A Comment: