Mjumbe kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Singida  Ndg Ahmed Misanga ambae pia ni mratibu wa shughuli za wazazi ikungi  ametoa Vifaa Vya ujenzi wa nyumba ya Mtumishi wa Jumuiya hiyo

Misanga Ametoa Vifaa hivyo  alipo tembelea na kujionea maendelo ya ujenzi huo.

"Nimetoa vifaa hivii ikiwa ni muendelezo wa Michango yangu katika  ujenzi wa nyumba ya Mtumishi wa wazazi  wilayani ikungi leo nimeleta Saruji , nondo , pesa ya ufundi kwa ajili ya kufunga lentha katika jengo hili" Misanga

" Pia tutaendelea kutoa michango yetu ili jengo hili liweze kukamilika kwa wakati na mtumishi aweze kuingia ndani,"

" Na tunamipogo wa kununua fenicha za ndani ili mtumishi akijaa  aje na mabegi  tu ili asipate tabu siku ya kuhama kama atakuwa amepata uhamisho wa kwenda mkoa mwingine,".

Huku katibu wa Jumuiya ya  wazazi walaya ya ikungi Bi HAWA GIDABUDAYI ameshukuru Mjumbe kamati ya Utekelezaji Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Singida  Ndg Ahmed Misanga kwa kujitowa kwake kwa ajili ya jumuiya hiyi kwa kutoa Vifaa vya  ujenzi wa nyumba hiyo ya  mtumishi.

" Kwani hili zoezi la kujenga nymba za watumishi ni agizo la kutoka makao makuu na sisi tumeadha kulitekeleza kwa vitondo na kwa sasa tupo hatua ya Kufunga Lentha paka ifikapo mwezi wakumi kila kitu kitakuwa kimekamilika na mtumishi ataingia ndani," Amesema 

Huku mwenezi wa chama cha mapinduzi wilaya ikungi Ndugu .NASSORO ISSAH Amesema chama kinawajubu wa kusimamia jumya zake ili ziweze kutimiza malengo yake.

 "Hizi nyumba zitasaidia sana watumishi wetu wanaokuja huku wilayani kwani akifika tu  anasehemu ya kulala, namini atafnyakazi zake kwa utulivu na kwa umakini kwasababu anasehemu ya uhakuka ya kuishi,".

" Sasa mtumishi wa wilaya ya ikungi akae tayari kuhamia baadaa ya lentha tunakwenda kupaua na kumalizia nyumba hiyo, " Ameongeza






Share To:

Post A Comment: