Na Mapuli Kitina Misalaba

Ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Shinyanga kwa kushirikiana na viongozi mbalimbali, wadau na wananchi leo asubuhi Aprili 25,2024 wamefanya usafi wa mazingira na kupanda miti 650 katika eneo la Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Miaka 60 ya muungano wa Tanganyika na Zanziber.

 Mgeni rasmi katika shughuli ni katibu tawala wa Wilaya ya Shinyanga Bwana Said Kitinga akimwakilisha mkuu wa Wilaya ya Shinyanga.

Pamoja na mambo mengina Bwana Kitinga ameikumbusha jamii kuendelea kupanda miti katika maeneo yao kama sehemu ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

Pia ametoa wito kwa watanzania kuendelea kushikamana na kushirikiana ili kuendeleza amani na usalama nchini.

Amesema ni vema watanzania kuendelea kushikamana  na kushirikiana katika shughuli mbalimbali za maendeleo ili kuendelea kuimarisha umoja na usalama wa taifa.

Afisa maliasili na mazingira wa Manispaa ya Shinyanga Ezra Manjerenga amesema miche ya miti 650 imependwa leo kama sehemu ya maadhimisho ya miaka 60 ya muungano wa Tanganyika na Zanziber ambapo amesema zoezi hilo ni endelevu.

Kwa upande wake Mganga mfawidhi wa Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga Dkt. Pierina Mwaluko ameahidi kuisimamia miti hiyo ili iweze kuleta matokeo chanya.

Baadhi ya wananchi na viongozi mbalimbali ambao wameshiriki shughuli ya upandaji miti wameeleza wataendelea kuunga mkono kampeni ya upandaji miti katika jamii ambapo pia  wameahidi kuendeleza amani na umoja wa  taifa hili.

Ofisi ya mkuu wa Wilaya ya Shinyanga kwa kushirikiana na viongozi mbalimbali, wadau na wananchi imefanya usafi wa mazingira na kupanda miti katika Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga ikiwa ni sehemu ya maadhimisho Miaka 60 ya muungano wa Tanganyika na Zanziber.

Kauli mbiu ya maadhimisho Miaka 60 ya muungano wa Tanganyika na Zanziber Mwaka huu inasema “TUMESHIKAMANA, TUMEIMARIKA KWA MAENDELEO YA TAIFA LETU”.

TAZAMA PICHA HAPA CHINI Shughuli ya upandami miti ikiendelea katika eneo la Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga leo Aprili 25,2024 ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya Miaka 60 ya muungano wa Tanganyika na Zanziber.

 

Share To:

Misalaba

Post A Comment: