Na John Walter-Manyara

Mwenyekiti wa  Umoja wa wanawake Tanzania (UWT) Mary Chatanda  amekabidhi Misaada  Mbalimbali  kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu ( Sera ,Bunge na Uratibu ) Mhe Jenista Mhagama walioathirika na Mafuriko wilaya ya Hanang' mkoani Manyara.

Chatanda amesema msiba huo mzito umeshtua Taifa na kwamba Umoja wa wameamua kujikusanya kwa Umoja wao kupeleka Misaada hiyo ambayo itasaidia wahanga.

"Sisi tulikuwa Rufiji kwenye Tamasha la Kumuenzi Bibititi Mohamed, lakini tukapata taaharifa hii na baadae tukaona kwenye  Vyombo mbalimbali vya Habari  tukasema kweli hali ni mbaya ndivyo  tukaketi na kamati yangu ya Utekelezaji tukaamua tuje na hiki  kidogo kwa ajili ya kurejesha tabasamu  kwa watu ambao wamepata shida hii "Amesema Chatanda.
Share To:

Post A Comment: