NA DENIS CHAMBI,  TANGA.

TAASISI ya Umoja wa  amani Kwanza  imempongeza Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama  Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kudumisha,   kusimamia na kuboresha misingi ya  amani kwa Taifa  ambayo imekuwa ni kielelezo kwa mataifa mbalimbali hususani ndani ya Africa.

Pongezi hizo wamezitoa leo December 16 mkoani Tanga katika  hafla iliyoambatana na kumpongeza rais wa taasisi hiyo Dkt  Wilson Munguza  kwa kutunukiwa cheo cha udaktari  na rais  wa amani kwanza Afrika Mashariki iliyotolewa hivi karibuni na Rais wa Uganda Yoweri Museveni.

Akimwakilisha Mkuu wa mkoa wa Tanga katika hafla hiyo ,  Mkurugenzi wa Halmashauri jiji la Tanga  Said Majaliwa ameipongeza taasisi hiyo kwa jitihada inazozifanya kwa kuvisaidia vyombo vya Ulinzi na Usalama katika kutekeleza na kusimamia majukumu yake ya kutoa elimu kwa jamii kuhusu umuhimu wa amani kwa Taifa  ambayo huchochoea maendeleo  kupitia nyanja mbalimbali.

Majaliwa amesema taasisi hiyo isiyokuwa ya kiserikali  itaendelea kupata ushirikiano wa hali na mali  kutoka serikalini katika kutekeleza majukumu yake ya kusimamia na kuilinda amani kwa Taifa ambayo imekuwa ikiwavutia wawekezaji katika maeneo mbalimbali  hapa Nchini.

Awali akizungumza  rais wa  Umoja wa amani kwanza Dkt Wilson Munguza amesema wataendelea kuwa msaada kwa vyombo vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha amani inakuwepo  na katika kuhakikisha wanawafikia watanzania wote wana malengo ya kufika hadi ngazi ya kata ili kutoa elimu na kusisitiza uzalendo kwa Taifa.

Aidha Dkt. Munguza ameiomba Serikali kuwashika mkono katika kutimiza lengo lao la kujenga chuo cha amani katika wilaya ya Handeni mkoani  Tanga kinachotarajiwa kuchukua wanafunzi kutoka ndani na nje ya Afrika mashariki.

" Ombi la taasisi kwa serikali ya  mkoa  wa Tanga  tunaomba kuelekea  lengo letu la kujenga chuo cha Amani  katika wilaya ya Handeni tunaomba  kupelekewa Buldoza  litakalosaidia kusafisha eneo  ambalo tunatarajia kujenga chuo hicho ambacho kitachukua wanafunzi wa kutoka ndani ya Nchi za Afrika Mashariki" alisema Dkt Munguza .

Akitoa salamu za jeshi la polisi kwa niaba ya kamanda wa mkoa wa Tanga ,  mkuu wa kitengo cha  Polisi jamii kamshina  msaidizi wa Polis  ACP  Yohana Mjengi ameipongeza taasisi hiyo kwa kazi wanazoendelea kuzifanya wakishirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha amani inaendelea kuwepo.

Aidha kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka amewataka wananchi kuchukua tahadhari na kuwa mabalozi wa amani katika kuwavumbua wahalifu sambamba na kuwataka madereva na wanatumia vyombo vya usafiri kuzingatia usalama barabarani ili kuepukana na matukio ya ajali ambazo zimekuwa zikigharimu maisha ya watu na mali zao.

"Tumetika ofisini kwenda  mpaka kwenye vijiji vitongoji na hata mitaa kwaajili ya kuongeza ulinzi shirikishi niwapongeze sana umoja wa amani kwanza  kwa kutambua umuhimu wa amani  sisi Polisi na wao majukumu yetu yanafanana  tumekuwa tukishirikiana  nao mara kwa mara  katik kutoa elimu ya kuimarisha amani  maendeleo yeyote pasipo kuwa na amani  hayawezi kuja" alisema ACP Mjengi.

"Jeshi la Polisi linawataka wananchi wote kuimarisha ulinzi na usalama hasa katika kipindi  hiki kuelekea  mwisho wa mwaka  kuhakikisha tunakuwa mabalozi wa amani na kwa upande wa madwreva kuzingatia sheria za usalama barabarani ,  wananchi wachukue tahadhari za kiusalama  hasa tunapokuwa kwenye mikusanyiko" alisisitiza.

Taasisi hiyo ya Amani Kwanza  ambayo ilianzishwa mwaka 2018 ikiwa na wanachama 14  inaendelea kukua ambapo  sasa imeweza kufikisha zaidi ya wanachama 5, 000 ikiwa ipo katika mikoa yote ya Tanzania.


rais wa Umoja wa amani kwanza Tanzania Dkt Wilson Munguza  akizungumza katika hafla hiyo

Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Tanga Said Majaliwa akimwakilisha mkuu wa Mkoa wa Tanga Waziri Kindamba katika hafla ya kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyofanyika leo December 16,2023 katika Hotel ya Panoli jijini Tanga ikiwa imeandaliwa na Umoja wa Amin kwanza.
Mkuu wa kitengo cha Polis jamii mkoa wa Tanga ACP Yohana Mjengi akizungumza katika hafla hiyo ikiwa amemwakilisha kamanda wa Jeshi la Polis mkoa wa Tanga.


Share To:

Post A Comment: