Kaimu Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU ) Mkoa wa Singida, Sipha Mwanjala akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kwa kipindi cha Julai-Septemba 2023 katika kikao kilichofanyika Oktoba 27, 2023.
Kikao na waandishi wa habari na maofisa wa TAKUKURU Mkoa wa Singida, kikifanyika.

Kikao kikiendelea.

.........................................................


Na Dotto Mwaibale, Singida

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU),Mkoa wa Singida imeokoa Sh. 54,087,750.58 zilizotokana na wazabuni kutowasilisha kodi ya zuio Mamlaka ya Mapato,Tanzania (TRA) na kupeleka vifaa pungufu katika miradi mbalimbali.

Hayo yamebainishwa Oktoba 27, 2023 na Kaimu Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Singida Sipha Mwanjala wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kwa kipindi cha Julai-Septemba 2023.

Alisema TAKUKURU Mkoa wa Singida kwa kipindi cha Julai –Septemba 2023 kwa upande wa uzuiaji rushwa walifuatilia utekelezaji wa miradi kumi na tatu yenye thamani ya zaidi Sh.Bilioni 5 katika sekta ya Elimu na Barabara na kuwa ilijumuisha miradi ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa
Taifa kwa fedha zilizotolewa na Serikali Kuu.

Alisema miradi mitatu iliyofuatiliwa yenye thamani ya Sh. Bilioni1.4 ilikutwa na mapungufu mbalimbali ambapo walitoa ushauri ili kukabiliana na mapungufu hayo. Alitaja baadhi ya mapungufu hayo ni kupeleka vifaa pungufu katika miradi tofauti na madai aliyowasilisha au fedha alizolipwa.

Akizungumzia kuhusu chambuzi za mifumo alisema katika kipindi tajwa TAKUKURU ilifanya chambuzi saba za mifumo ili kubaini mianya ya rushwa iliyopo katika maeneo hayo na kisha
kushauri namna ya kuiziba na kuwa Warsha saba zilifanyika kwa ajili ya kujadili mianya ya rushwa
iliyobainika katika chambuzi zilizofanyika na kuweka mikakati ya kuziba mianya ya rushwa iliyobainika.

Aidha, Mwanjala alisema TAKUKURU Mkoa wa Singida iliendelea na utekelezaji wa Programu ya TAKUKURU RAFIKI kwa kufanya vikao 18 na wadau katika kata 18 ambapo wadau waliibua kero 175.

Alisema kero zilizotatuliwa mpaka sasa ni 125 na kero 50 zinaendelea kupatiwa ufumbuzi.
Akielezea upande wa elimu kwa umma alisema TAKUKURU Mkoa wa Singida iliwaongezea wananchi uelewa wa masuala ya rushwa kwa kufanya Semina 34 kwenye makundi mbalimbali
wakiwemo watumishi wa umma.

Alisema pia walifanya mikutano ya hadhara 17,maonesho 7, kutembelea na kuimarisha klabu za wapingarushwa 43 katika Shule za Msingi, Sekondari na Vyuo Akizungumzia suala la uchunguzi na mashitaka alisema malalamiko 76 yalipokelewa, ambapo malalamiko 52 yalihusu
vitendo vya rushwa na malalamiko 24 hayakuhusu rushwa.

Alisema malalamiko 52 yaliyohusu rushwa uchunguzi wake unaendelea katika hatua mbalimbali na
malalamiko 24 ambayo hayahusiani na rushwa walalamikajiushauri.

Alisema katika kipindi hicho kesi 10 zilifunguliwa mahakamani,kesi 13 ziliamuliwa, kesi 8zilishinda.

Akizungumzia mikakati ya utendaji kazi waliojiwekea kwa robo ya pili ya mwaka 2023/2024 ya kuanzia mwezi ni kufuatilia matumizi ya fedha za Serikali zinazoelekezwa Mkoa wa Singida
kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo na Kuendelea kuwaongezea uelewa wananchi kuhusiana na masuala ya rushwa ili wananchi washiriki kikamilifu katika kuzuia vitendo
hivyo hasa katika miradi ya maendeleo inayoendelea katika maeneo yao, Kuendelea na utekelezaji wa Programu ya TAKUKURU – Rafiki.

Mwanjala alitoa wito kwa kusema kuwa TAKUKURU Mkoa wa Singida inatoa RAI kwa wananchi wote kujiepusha na vitendo vya rushwa na kushiriki kikamilifu kuzuia vitendo vya rushwa vinavyotokea katika maeneo mbalimbali ya kutolea huduma za kijamii. Pia, kuzuia vitendo hivyo hasa
katika miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika maeneo yao,na kutoa taarifa za vitendo vya rushwa kwa kufika Ofisi za TAKUKURU Mkoa wa Singida na Wilaya za Iramba,Ikungi,Mkalama na Manyoni.

Mwanjala alitaja njia nyingine ya kutoa taarifa hizo ni kupiga simu ya Mkuu wa TAKUKURU Mkoa na wakuu wa TAKUKURU wa Wilaya kwa namba RBC –Singida 0738150208, DBC -Mkalama 0738150 212, DBC - Ikungi 0738150213, DBC -Iramba 0738150 210 na DBC - Manyoni 0738150 211 na
akaomba wananchi kutoa ushirikiano kwenye uchunguzi na kushiriki kutoa ushahidi Mahakamani.
Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: