Mshauri Mkuu wa masuala ya kijamii kutoka Kampuni ya Shell Tanzania, Msumis M'bena akizungumza wakati akifunga mashindano yaliyo wakutanisha wanafunzi wanaosoma masomo ya Sayansi kutoka Shule za Sekondari 15 za Mkoa wa Lindi yaliyofanyika Oktoba 2, 2023 mkoani humo.
.........................................
Na Said Hauni, Lindi.
TAASISI ya Young Scientits Tanzania (Yst)
imewakutanisha wanafunzi wanaosoma masomo ya sayansi katika Shule za Sekondari
(15) za Mkoa wa Lindi, lengo likiwa kuonyesha uwezo wa kimawazo katika ugunduzi
na bunifu mbalimbali zitakazowawezesha kusaidia Jamii na Taifa,
Makutano hayo yaliyokuwa imeshirikisha Sekondari
(15) Halmashauri za Kilwa, Liwale, Nachingwea, Ruangwa, Mtama na Manispaa ya
Lindi,umefanyika ukumbi wa Sekondari ya
Wamasharaf mjini Lindi.
Akitoa taarifa wakati wa kufunga kikao cha
makutano hayo,mwakilishi wa taasisi hiyo, Botgas Kamugisha alisema la
mashindano hayo ni kuwawezesha wanasayansi chipukizi kukuza bunifu walizonazo
kwa ajili ya kusaidia jamii na Taifa.
Kamugisha alisema katika mashindano hayo
sekondari (15) kutoka Halmashauri za Kilwa,Liwale, Nachingwea ,Ruangwa.Mtama na
Lindi Manispaa zimefanya vizuri katika Project zao kubuni mambo mbalimbali.
Alisema kati ya shule hizo zilizofanya vizuri ni
mbili za Mkowe,Wilaya za Ruangwa na Kivinje Kilwa na kuwakilisha Mkoa wa Lindi
katika madhindano yatakayofanyika Dar es Salaam, Oktoba 17,2023.
Mwakilishi
huyo alisema Sekondari ya Kivinje imeibuka mshindi kwa Project yao kuibua
kinyesi cha wadudu waitwao Youth Breck Soja kutengenezea mbolea,wakati Shule ya
Mkowe kugundua dawa ya kutibu maradhi ya tumbo kwa kutumia magome ya mti wa
mwembe.
Naye, mshauri mkuu wa masuala ya kijamii kutoka
Kampuni ya Shell Tanzania,Msumis M'bena alisema kampuni hiyo inafadhili mradi
huo kuanzia mwaka 2913 lengo likiwa ni kuboresha masomo ya sayansi kwa shule za
sekondari,hali inayowasaidia kuwa wabunifu na watafiti wazuri.
Akifunga kikao cha makutano ya mashindano hayo,
Afisa Elimu Mkoa wa Lindi, Joseph Mabeo amewataka wanafunzi kupenda kusoma
masomo ya sayansi,ikizingatia Tai linahitaji wataalamu wa kutosha kwa lengo la
kusaidia nchi.
Mabeo amesema kutokana na umuhimu huo Serikali
inaendelea kuweka msisitizo na fedha za kuongeza ujenzi wa Shule na maabara.
"Mwaka huu Serikali imeupatia Mkoa wetu wa
Lindi Sh,5.0 bilioni kujenga Sekondari kwa masomo ya sayansi pekee"Alisema
Mabeo.
Wakizungumzia ushindi walioupata,Hadija Mohamedi
na Mustapha Omari, Kivinje Sekondari na Gabliel Daniel na Mary Agustine wa
Shule us Mkowe wanaishukuru Taasisi ya YST kuandaa mashindano hayo kwani
yanawasaidia kufikiri katika gunduzi wanazozifanya, huku wanaamini kufikia
malengo yao.
Post A Comment: