Na Denis Chambi, Tanga.

KAMATI ya Bunge  ya elimu ,utamaduni  na michezo imelipongeza shirikisho la mpira wa miguu Tanzania 'TFF' kufwatia uwekezaji unaoendelea katika ujenzi wa mradi wa  vituo viwili vikubwa vya michezo  vilivyopo  Mnyanjani Tanga na Kigamboni mkoani Dar es salaam huku ikiiomba serikali kuona haja ya kujenga vituo vingine Kama hivyo mikoani.

Miradi hiyo mikubwa  inayotekelezwa  hapa nchini   ambapo kwa Tanga  ulianza kutekeleza rasmi 2020 na kukabidhiwa februry 2023 ukiwa tayari kwa awamu ya kwanza umekamilika katika ujenzi wa viwanja viwili hosteli pamoja na jengo la utawala .

Mara baada ya kukamilika TFF imedhamiria kuwekeza katika soka la vijana wa kike na wa kiume wenye umri kati ya miaka 4-23 ambapo vijana wa kike  watakaopatikana katika mikoa mbalimbali hapa nchini  wataweka kambi Kigamboni Dar de Salam huku wakiume wakiwa Mnyanjani jijini Tanga wakinolewa tayari kwajili ya michauano mbalimbali  ya kuliwakilisha Taifa.

Akizungumza mara baada ya kutembelea mradi huo  leo September 9, 2023 akiwa pamoja  na wajumbe wake mwenyekiti wa kamati ya Bunge  ya elimu, utamaduni na michezo Husna Sekiboko ameipongeza serikali kwa mapinduzi makubwa inayoyafanya kupitia sekta ya michezo hususan katika mradi huo ambao unakwenda kukuza vipaji vya wachezaji ,makocha ambao ni hazina ya Taifa la baadaye.

Ameipongeza TFF kwa kuendelea kusimamia maendeleoya mpira wa miguu  hapa nchini hasa katika kipindi hiki ambapo timu za Taifa zinaendelea kufanya vizuri kimataifa ikikubukwa kuwa ni siku chache tu zimepita tangu  Taifa Stars ilivyofuzu kwenda kucheza michauano ya Afcon 2024 nchini Cameroon.

Sekiboko ambaye pia ni Mbunge wa viti maalum mkoa wa Tanga alilisisitiza shirikisho la mpira miguu Tanzania 'TFF' kuendelea kuimarisha mahusiano baina yao na  wizara ya michezo ili kuweza kusimamia  na kufanikisha maono na mipango ya serikali katika kutaka kuleta maendeo kupitia sekta hiyo.

"Kwa niaba ya kamati hii  nimpongeze sana Rais Samia Suluhu Hassan  kwa nguvu kubwa anayoitumia katika kuwezesha sekta ya michezo tumeshuhudia katika michauano ya vilabu mbalimbali lakini hata katika timu zetu za Taifa amewekeza fedha nyingi na ameonyesha   nia ya dhati ya kutaka kuendelea michezo nchini ". amesema Sekiboko.

Niwapongeze Sana TFF kwa mipango mikubwa mnayoifanya hadi leo  tunaona timu zetu za Taifa zinafanya vizuri   niwaombe sana kudumisha mahusiano  ni jambo la msingi sana , mnafanya kazi nzuri sana sio tu katika miradi ya ujenzi lakini hata  katika kuzinoa timu zetu za Taifa tumeona sasa Tanzania inavyunja mwiko  kwa kutoka nje ya mipaka na kufanya vizuri tunawapongeza  sana endeleeni na jitihada hizo za kuhakikisha kwamba timu zetu za Taifa zinaendelea kufanya vizuri" aliongeza.

Akizungumza naibu  waziri wa  wizara ya Sanaa utamaduni na michezo Hamis Mwinjuma 'Mwana FA' amesema kuwa wizara itaendelea kuhakikisha michezo yote hapa nchini inapewa kipaumbele na kupitia vituo hivyo itakuwa ni njia bora ya kuwapata wachezaji wenye vipaji watakaokuja  kushindana katika medani  za kimataifa.

"Tunaona umuhimu wa kufanya mambo makubwa namna hii kwa sababu tunaamini vituo hivi maendeo makubwa ya mpira wa miguu hapa nchini, moja ya mipango ambayo tunayo kwa sasa hivi Kama serikali ni kujenga kituo kikubwa cha michezo ambacho kitasaidia kufundishia walimu wanaokuja kufundishia michezo huku mashuleni na vyuoni na serikali tunahakikisha kwamba maendeo yanaendelea kufanyika" alisema Mwana FA.






Share To:

Post A Comment: