Afisa Mfawidhi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mkoani Tanga Kapten Christopher Shalua akizungumza leo wakati wa kikao cha wadau wa taasisi mbalimbali wanazoshirikiana nao kufanya kazi za usafiri majini ili kujenga mahusiano na kukumbushana baadhi ya wajibu wao.


Afisa Mfawidhi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mkoani Tanga Kapten Christopher Shalua akizungumza leo wakati wa kikao cha wadau wa taasisi mbalimbali wanazoshirikiana nao kufanya kazi za usafiri majini ili kujenga mahusiano na kukumbushana baadhi ya wajibu wao.


Afisa Mfawidhi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mkoani Tanga Kapten Christopher Shalua akizungumza leo wakati wa kikao cha wadau wa taasisi mbalimbali wanazoshirikiana nao kufanya kazi za usafiri majini ili kujenga mahusiano na kukumbushana baadhi ya wajibu wao.
mmoja wa wadau hao akiuliza swali katika kikao hicho

Sehemu ya washiriki wa kikao hicho


Na Oscar Assenga,Tanga

SHIRIKA la Wakala wa Meli Tanzania (TASAC) wamekutana na wadau wa taasisi mbalimbali wanazo shirikiana nao kufanya kazi za usafiri majini ili kujenga mahusiano na kukumbushana baadhi ya wajibu wao.

Hayo yalibainishwa leo na Afisa Mfawidhi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) Mkoani Tanga Kapten Christopher Shalua wakati wa kikao hicho cha pamoja ambapo alisema kwamba wajibu wao ambao unawataka kuyatimiza majukumu yao ya kisheria.

Kapteb Shalua ambaye pia ni Afisa Mkaguzi wa vyombo vya majini Mkoani Tanga wajibu huo unawataka kuhakikisha usafiri wa maji unakuwa ni salama pamoja na uwepo wa utunzaji wa mazingira

“Kwa hiyo tulikutana na taasisi mbalimbali ikiwemo TPA,Marine Park ambao ni wabia wenzetu katika utunzaji wa mazingira ya bahari ,Afya,Maafisa Uvuvi kwa ajili ya kujadiliana na kusikiliza maoni kutoka kwao namna ya kuweza kuboresha mashirikiano yao ili kila taasisi waweze kufikia malengo yaliyokusudiwa”Alisema

Hata hivyo alisema malengo hayo yatasaidia kuhakikisha usafiri wa majini au shughuli za majini zinatendeka kwa hali ya usalama na amani lakini pia pia kuwepo na utekelezaji wa sheria.
Share To:

Post A Comment: