Mwenyekiti wanchama cha mapinduzi CCM Mkoa wa Iringa Daud Yassin akiongea na madereva bajaji wa mkoa wa Iringa umuhimu wa kusomea udereva na kupata cheti cha udereva



Na Fredy Mgunda, Iringa.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa,Daud Yasin amemwaga neema kwa madereva bajaj watakao kubali kuingia darasani kupata mafunzo ya udereva na usalama barabarani.


Amesema kwa wale 100 wa kwanza kupata mafunzo hayo atawalipia leseni na lengo kubwa kwake ni kupunguza makosa ambayo huchangia ajali za barabarani.


Ndugu Yassin alikuwa akiongea kwenye mkutano wa madereva bajaj uliofanyika kwenye ukumbi wa CCM Mkoa wa Iringa pia, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, *Ndugu Halima Dendego* alitumia nafasi yake kuwafunda watii sheria bila shuruti.


"Wale 100 wa kwanza watakao jifunza vizuri na kuelewa nitawalipia leseni, lakini muhimu kufuata sheria," amesema *Ndugu Yasin*


Mwenyekiti huyo wa CCM Mkoa wa Iringa aliwaambia kazi ya chama hicho ni kuisimamia Serikali lakini, madereva hawana budi kutii sheria bila shuruti.


Alitumia nafasi hiyo kutoa salamu za Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan akiwasihi vijana hao kuendelea kumuunga mkono.

Share To:

mwangaza wa hbari

Post A Comment: