Uongozi wa umoja wa wanawake Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi UWT Mkoa wa Arusha  umefanya kikao  cha baraza la  mkoa ili kutoa utatuzi  wa changamoto walizokutana nazo katika ziara ya siku tatu iliyofanyika katika wilaya  ya Arumeru  mkoani humo ikiwemo   sekta ya afya ,ukatil  kijinsia na mikopo kwa wanawake. 

Miongoni  Mwa changamoto  zilizotolewa fafanuzi ni  pamoja na Zahanati ya  kata ya Maruvango   kukosa  vifaa tiba  na vitanda vya kujifungulia  wakina mama wajawazito  naseikali imekwisha andaa bajeti katika kutatua changamoto  hiyo katika vituo vyote vya  afya ambavyo vimekuwa na changamoto  kubwa.  amesema  DMO  Mganga mkuu wa wilaya ya  Arumeru Dr Maneno Focus 

Pia amesema  serikali unania njema na watu wake hususani kwa wakinamama kwa  kuendelea  kupambana na vifo vya mama na mtoto kwa kuboresha huduma  bora ya afya  

Afsa maendeleo  ya jamii wilaya ya meru frola  Msilu  amewataka maafisa maendeleo ya jamii wakata kuwana ushirikiano wakutosha  katika kufanya kazi huku akiwataka wakina mama ambao vikundi   vyao havirejeshi mikopo  kwa wakati warudishi ili wengine waweze

Ili kupinga swala la ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto Halmashauri ya Wilaya ya Arumeru  imeanzisha  vikundi mbalimbali  mashuleni vinavyotoa elimu  kwa wanafunzi  itakayo saidia kupunguza  ukatili wa kijinsia  kwa watoto huku wakishirikiana na wazazi kiwachukukia hatua wahusika. Amesema  frola Msilu. 

Nae Mkuu wa   wilaya  ya Arumeru Emmanuela Mtatifikolo Kaganda ameupongeza  uongozi wa UWT  kwa kazi wanazozifanya kwa manufaa ya wananchi huku akiahidi kuzifanyia kazi changamoto  zote zilizotolewa  na wananchi kufikana na fedha zilizotolewa na serikali katika sekta  ya Elimu bilion moja na million miasaba arobaini,  afya bilioni mbili na milioni miasaba na mikopo  isiyo nariba bilioni moja na milioni  mia moja sabini na sita. 

Mwenyekiti wa UWT mkoa wa Arusha Flora Zelothe  akiwa Mgeni rasmi katika baraza hilo amezungumzia swala la ukatili  linazidi kukua Siku baada ya Siku hivyo juhudi zi nahitajika. 

"Ukatili wa kijinsia Umekuwa ukifanyika asilimia 66.6 majumbani hii inatokana na  wamama kuwa bize na kutafuta kipato mda mwingi wanakuwa  makzini na katika biashara wakirudi nyumbani usiku wakiwa wamechoka nakupelekea kukosa  mda wa kumkagua mtoto wake. 

Pia amewataka wanawake  kuhamasishana kugombea   nafasi mbalimbali  katika uongozi  ili kufanikisha jambo hilo ni lazima wanawake  wawe  na umoja kwa kushikamana na kupendana. 

Nae mwenyekiti  wa UWT  Wilaya hiyo  Juliet Maturu ameushukuru uongozi wa mkoa kwa kutembelea katika wilaya yake na kuwataka viongozi  wa ngazi zote kuanzia vijiji mpaka tarafa kufanya kazi kwa kushirikiana na kujitoa. 


Share To:

Post A Comment: