Na Denis Chambi, Tanga.

TAASISI ya Masjid Muzdalfa kwa kushirikiana na Waterfall Charity UK kutoka nchini Uingereza imekabidhi Nyumba 6 kwa familia  za watoto yatima wilayani Tanga hii ikilenga  kuwaondoa katika Mazingira magumu.

Taasisi hiyo  inayoongozwa na Mkurugenzi wake Al Haji Twaha Omari Tawakal  ambayo inamiliki shule ya msingi ya Muzdalfa Mwakidila ikishirikiana na waterfall Charity  UK inawalipia ada  wanafunzi yatima na wasiojiweza 170 shilingi laki nne (400, 000 ) kila mmoja kwa mwaka  pamoja na kuwawezesha  mahitaji muhimu ya binadamu ikiwemo chakula na maradhi.

Akizungumza wakati wa hafla ya kukabidhi nyumba hizo katibu tawala  msaidizi wilaya ya Tanga Mussa Machunda kwa niaba ya  mkuu wa wilaya hiyo amewapongeza Muzdalfa pamoja na Waterrfall charity kwa kuyatazama makundi hayo muhimu  wakiunga mkono jitihada za kusogeza karibu na kutoa huduma mbalimbali kwa jamii.

"Niwapongeze sana kwa kazi kubwa ambayo mnaifanya,  tunafahamu kuwa kazi ya kutoa huduma kwa jamii ikiwemo elimu,  maji,  afya  na nyinginezo ni kazi ya serikali lakini  nyinyi kama wadau mmeamua kuyasaidia kwenye maeneo kama hayo, kwani tunaona tatizo hili la watoto  yatima katika jamii sasa hivi limefanya baadhi ya watoto wengi kukosa wazazi hivyo kumfanya mtoto aishi kwenye mazingira magumu  na baadhi ya wazazi na walezi kushindwa kukidhi mahitaji kwa kweli hili ni jambo la kipekee na la kupongezwa"

"Katika mambo ambayo yanakubaliwa  na Mungu ni ibada za kuhudumia watu wasiojiweza  wakiwemo yatima na watoto wanaoishi kwenye  mazingira magumu, na ninyi mmeona hiyo ni fursa mkaamua kuwasaidia wayoto wetu na pengine watoto hawa huduma  hizi wasingezipata lakini na sisi wengine tupate fundisho kutoka kwa hawa wenzetu tunapojaaliwa kuwa na uwezo wa mali basi tuwakumbuke na wenzetu wahitaji  " alisema Machunda

Akitoa taarifa ya Masjid Muzdalfa  Fatuma  Mgunya amesema kuwa kwa kushirikiana na  Water fall  Charity wamefanikiwa kuchimba visima vya maji  zaidi ya 20 kwajili ya kuwasaidia wakazi wa maeneo mbalimbali kupata huduma ya maji huku wakitoa kiasi cha shilingi Million 40 kwajili  ya kuziwezesha familia zenye watoto yatima kujikimu kimaisha.

"Muzdalfa hutoa maji bure kwa wakazi wanaozunguka shule lakini pia kwa kushirikiana na  Wayerfall Charity tumechimba  visima zaidi ya 20 lakini pia  tumeweza kutoa  gedha taslimu  kwa hawa yatima  kwaajili ya kujikimu ambazo mpaka sasa  wameshagawiwa zaidi ya shilingi Million arobaini.

Pamoja na hayo taasisi hiyo ya Muzdalfa kwa kushirikiana na Water fall Charity imeweza kuwalipia   ada  wanafunzi 16 kati ya 36 waliofanya vizuri mitihani yao ya  darasa la saba  ambao wamejiunga kwenye  shule mbalimbali  za sekondari katika muhula wa masomo wa mwaka 20223.

Mwenyekiti wa wafadhili mkoa wa Tanga ambaye pia mwenyekiti wa taasisi ya " Wapenda Kheri Foundation" Ally  Masomaso amewapongeza na kuwashukuru wadau mbalimbali wakiwemo water fall Charity ambao wanashirikiana nao katika kusaidia jamii pamoja na mswala ya dini ikiwemo kujenga misikiti huku akizitaka taasisi zilizopo ndani ya Mkoa wa Tanga kuunganaa katika kuziwezesha jamii katika nyanja mbali mbali.

Aliongeza kuwa taasisi ya  Kheri Foundation ambayo inaunga mkono katika kusaidia jamii  za wahitaji katika nyanya mbalumbali tayari  imeshajenga nyumba nne  kwaajili ya  watoto yatima ndani wilaya ya Pangani pamoja na Misikiti ambapo bado wanaendeleza jitihada hizo.

"Tunawashukuru sana wafadhili wetu kutika nchi tofauti tofauti duniani wamekuwa wakitusaidia katika mambo mbalimbali ya kusaidia jamii pamoja na kujenga misikiti, taasisi ya Muzdalfa tunawashukuru sana kwa msaada huu wanajitahidi sana  kwaajili ya kuwasaidia mayatima tukipata taasisi kama hizi  na tukaungana iyakuwa ni jambo jema nia yetu sisi ni kuijenga Tanga iwe moja" alisema.

Baadhi ya wazazi na walezi walikabidhiwa  nyumba hizo  akiwemo Halima Cheo na Fatuma Ally  wameishuku taasisi ya Muzdalfa pamoja na Waterfall Charity UK kwa kuwawezesha makazi hayo ambapo awali wamekuwa wakipata changamoto mbalimbali ya maradhi.

"Namshukuru sana kwa kunipatia  hifadhi kama hii kwa kweli sikutegemea  Mungu mwenyewe ndiye atakayewalipa sina cha kuwalipa nitaishi na familia yangu , nashukuru uongozi wete wa Muzdalfa na Water  fall Charity kwa kutufanyia wema huu" walisema  






 

Share To:

Post A Comment: