Naibu Waziri wa Maendeleo ya jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalumu Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Mbeya ameanza ziara ya kikazi Wilaya ya Monduli Mkoani Arusha ukiwa ni muendelezo wa kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali.

Awali Mhandisi Maryprisca Mahundi amefika ofisi za Chama Cha Mapinduzi (CCM)Wilaya ya Monduli kwa ajili ya utambulisho.

Akiongea na uongozi CCM wa Wilaya ya Monduli Mheshimiwa Mhandisi Maryprisca Mahundi ameahidi kutekeleza majukumu kwa lengo la kumsaidia Mwenyekiti wa CCM Taifa ambaye pia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan.

Waziri na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Wanawake na Makundi Maalumu wanafanya ziara nchi nzima kukagua miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa mabweni ya wasichana katika vyuo vya Maendeleo ya jamii.












Share To:
Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

Post A Comment: