Na Denis Chambi, Tanga.
MWENYEKITI  wa Chama cha Demokrasia  na Maendeleo 
CHADEMA kanda ya Kaskazini Godbless Lema ameendelea kusimamia kauli yake
 aliyoitoa hivi karibuni kuwa shughuli ya madereva waendesha pikipiki 
maarufu kama Boda boda sio kazi badala yake inauwa nguvu kazi ya Taifa 
la kesho akisistiza kuwa bado kundi hilo ni janga lililopo hapa nchini 
wengi wakishindwa kuyamudu maisha wanayoishi na familiya zao. 
Lema
 ameendelea kusisitiza kauli hiyo akiwa mkoani Tanga march 20 , 2023 
katika mkutano wa hadhara ikikumbukwa kuwa mara tu alipowasili hapa 
nchini  january 2023 akitokea  Canada alikokuwa tangu mwaka 2020,  
ambapo mara baada ya kukutana na mamia ya wafuasi wa chama hicho mkoani 
Arusha aliizungumza na hatimaye kuibua baadhi ya viongozi wa vyama vya 
siasa pamoja na uongozi wa Bodaboda wakimtaka akanushe kauli yake na 
kutokuibize  kazi hiyo lakini bado ameonyesha  msimamo wake.
"Nasema
 sifuti kauli na leo tena  napigilia  msumari kuwa udereva boda boda sio
 kazi  ya maana na watu wanazidi kuwa masikini na hii inajenga ufukara, 
bodaboda zimeongeza vilema  na wajane  leo hii kuna watu 
wanapoteza ndugu zao na maisha kwa sababu ya ajali za boda boda ,  " 
alisema Lema
Aidha 
Lema ameeleza kuwa kuna athari ambazo zinaweza kujitokeza hapo baadaye 
kutokana na wazazi walezi na jamii kwa ujumla kushindwa kuwalea watoto 
katika maadili mema jambo ambalo linaweza kuchoche kushamiri kwa vitendo
 vya ukatili sambamba na kupoteza nguvu kazi ya Taifa.
"
 Watoto wengi wanaozaliwa sasa hivi hawalelewi na wazazi wao ipasavyo 
kama nyakati za wazee wetu  je! Hivi meangalia taifa hili baada ya miaka
 30 nchi itakuwaje nyie? ndio maana sasa hivi tunashangaa kuna tabia 
zinazuka umasikini umekuwa mkali kuwanyima  nafasi kwa wazazi 
kuwaangalia watoto" aliongeza Lema.
Awali
 akizungumza mjumbe wa halmashauri kuu ya CHADEMA Taifa Grace Kiwelu  
alimpongeza  Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kwa hatua aliyochukuwa ya 
kufungua  milango na kuridhia mashirikiano baina ya vyama vyote vya 
siasa pamoja na kuruhusu mikutano ya kisiasa  akisema kuwa licha ya hayo
 yote bado CHADEMA itaendelea kusimamia msimamo wake kuhubiri umuhimu wa
 kupatikana kwa katiba mpya.
"Niwashukuru
 sana viongozi wetu wa vyama viwili wa Kitaifa wa Chama Cha Mapinduzi 
'CCM'  na  Chama cha Demokrasia na Maendeleo 'CHADEMA' kwa kuleta 
maridhiano leo watanzania tunazungumza ,  tumekuwa kwenye lifungo cha 
miaka saba bila watanzania kuzungumza"
Mkutano
 huo uliofanyika katika viwanja vya  kata ya Msambweni ulihudhuriwa pia 
na aliyewahi kuwa Mjumbe wa halmashauri kuu Taifa wa Chama cha Mapinduzi
 'MNEC'.
Pamoja na 
hayo chama hicho kimtembulisha uongozi mpya wa CHADEMA ngazi ya wilaya 
ukiongozwa na Rashid Jumbe ikikumbukwa kuwa katika ziara ya mwenyekiti 
taifa  Freeman Mbowe aliyoifanya hivi karibuni mkoani Tanga aliuvua 
madaraka uongozi uliopo na kuwachagua wengine hii ikilenga hasa kuzidi 
kukiimarisha chama hicho kuanzia ngazi za chini.
Uongozi
 huo mpya unaoongozwa na aliyekuwa mwanachama wa ACT Wazalendo na ambaye
 baadaye kuhamia CHADEMA kwa sasa akikaimu nafasi ya mwenyekiti  , Khalid 
Hamza kaimu katibu,  Shaban Ngozi aliyeteuliwa kuwa  katibu mwenezi wa 
chama hicho, Zima Mohammed akikaimu nafaai ya baraza la wazee,   Zena 
Khamis kaimu mwenyekiti Bawacha,  Amos Chiluda Mwenyekiti wa wazee 
Selestin Kiria mweka hazina wa jimbo na wengine wengi waluokaimu nafasi 
zilizoachwa wazi mara baada ya mabadiliko kitoka uongozi uliopita.
Mjumbe wa halmashauri kuu ya chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Grace Kiwelu akizungumza katika mkutano huo.
Mwenyekiti wa CHADEMA (kushoto) mkoa wa Tanga akisalimiana na aliyewahi kuwa MNECwa chama cha mapinduzi CCM mkoa wa Tanga ambaye walimualika katika mkutano huo.
Uongozi mpya wa chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA wilaya ya Tanga uliotambulishwa rasmi katika mkutano wa hadhara wa mwenyekiti wa chama hicho kanda ya Kaskazini Godbless Lema uliofanyika mkoani Tanga March 20,2023.




Post A Comment: