Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba, akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Puma kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Januari 19, 2023 anayoendelea kuifanya ikiwa ni muendelezo wa ziara za kutembelea kila wilaya kwa ajili ya kusikiliza kero mbalimbali na kuzipatia ufumbuzi. Kushoto ni Katibu Tawala Wilaya ya Ikungi, Winfrida Funto na kulia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa wilaya hiyo, Mika Likapakapa. 

Na Dotto Mwaibale, Ikungi Singida

MKUU wa Mkoa  wa Singida Peter Serukamba ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa ameviagiza vyombo vya dola wilayani Ikungi kuchunguza matukio ya  uhalifu yanayodaiwa kuhusisha watoto wenye umri usio zidi miaka 15.

Serukamba alitoa agizo hilo Januari 19, 2023 baada ya  kuibuliwa na wananchi wa Kijiji cha Puma  wilayani  Ikungi katika mkutano wa hadhara ikiwa ni muendelezo wa ziara za kutembelea kila wilaya kwa ajili ya kusikiliza kero mbalimbali na kuzipatia ufumbuzi.

Kero hiyo iliibuliwa na mwananchi wa kijiji hicho Joramu Zakaria ambaye alisema vitendo hivyo vya uhalifu vimekithiri katika eneo hilo kwa kiwango cha mtu kutokuwa na uhakika wa kuamka salama.

Mwenyekiti wa kijiji hicho Samwel Mbiaji alikiri kuwepo vitendo hivyo na kuwa walifanya msako kwa kushirikiana na polisi na kuwa asilimia 75 ya waliokamatwa walikuwa na umri  umri usiozidi miaka 15 ambao waliachiwa.

"Tukiwaita wazazi wao wanatuambia tufanye tunavyotaka wao wamewashinda sasa mkuu sisi tufanyeje" alisema Mbiaji.

Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Ikungi, Suzana Kidiku aliahidi kulishughulikia suala hilo kwa kuwashirikisha maafisa wa ustawi, viongozi wa kijiji na kuwa wanatarajia kufanya msako wa kuwabaini wahalifu hao.

Kero nyingine iliyoibuliwa katika mkutano huo ni ile iliyotolewa mfanyabiashara wa viazi Fatuma Ramadhani ambaye aliomba kuwepo kwa soko la uhakika kwa kuwa hivi sasa wanauza bidhaa hiyo maeneo yasiyo rasmi na kusababisha kuchafua mazingira.

Pia alilalamikia utozwaji wa ushuru mara mbili unaofanyika eneo la Kintinku baada ya kutozwa wa awali wanapotoka katika kijiji hicho.

Kufuatia kero hiyo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Justice Kijazi alisema wanatarajia kujenga soko la kisasa katika kijiji hicho ambalo litaondoa changamoto hiyo.

Akizungumza baadaya kupokea kero hizo  Serukamba amewataka viongozi na watumishi wa Serikali wilayani humo kutekeleza wajibu wao kwa kufanya kazi kwa bidii ya kutoa huduma kwa wananchi.

Alisema jambo kubwa aliloliona baada ya kusililiza kero hizo ni baadhi ya viongozi kushindwa kutekeleza wajibu wao ipasavyo na akawaomba viongozi hao kwenda katika Tarafa na Kata kufanya kazi hiyo na kuacha tabia ya kukaa ofisini.Mkuu wa Polisi Wilaya ya Ikungi (OCD), Suzana Kidiku akipiga saluti kwa Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba (Aliye kaa meza kuu kushoto) ikiwa ni kuonesha utii baada ya kutakiwa kushughulikia madai ya watoto kuhusishwa na vitendo vya uhalifu.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Peter Serukamba akisisitiza jambo kwenye mkutano huo. Kushoto ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Ikungi, Winfrida Funto.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Ikungi, Mika Likapakapa, akizungumza kwenye mkutano huo.
Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Singida, Msama Msama akizungumza kwenye mkutano huo.
Wakina mama wa Kijiji cha Puma wakiwa kwenye mkutano huo.
Katibu wa CCM Wilaya ya Ikungi, Stamili Dendego akizungumza kwenye mkutano huo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi, Justice Kijazi akiteta jambo na mkuu wa mkoa wakati wa mkutano huo.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Ikungi, Winfrida Funto akizungumza kwenye mkutano huo.
Taswira ya mkutano huo.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye mkutano huo.
Afisa Kilimo, Umwagiliaji  na Ushirika wa Wilaya ya Ikungi, Gurisha Msemo akizungumza kwenye mkutano huo.


Mfanyabiashara ya viazi vitamu, Fatuma Ramadhani akitoa kero yake kwa mkuu wa mkoa.
Mkazi wa Puma, Joramu Zakaria akitoa kero yake kwenye mkutano huo.
Afisa Ardhi wa Wilaya ya Ikungi, Ambros Ngonyani akizungumza kwenye mkutano huo.
Mkutano ukiendelea. 


Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: