Watumishi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) wakicheza drafti katika Bonanza la Michezo kwa wafanyakazi wa Shirika hilo lililofanyika leo Septemba 17,2022 katika viwanja vya Chuo cha Ardhi Jijini Dar es Salaam.Watumishi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) wakicheza bao katika Bonanza la Michezo kwa wafanyakazi wa Shirika hilo lililofanyika leo Septemba 17,2022 katika viwanja vya Chuo cha Ardhi Jijini Dar es Salaam. Watumishi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) wakicheza mpira wa miguu katika Bonanza la Michezo kwa wafanyakazi wa Shirika hilo lililofanyika leo Septemba 17,2022 katika viwanja vya Chuo cha Ardhi Jijini Dar es Salaam. Watumishi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) wakicheza Volley ball katika Bonanza la Michezo kwa wafanyakazi wa Shirika hilo lililofanyika leo Septemba 17,2022 katika viwanja vya Chuo cha Ardhi Jijini Dar es Salaam. Watumishi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) wakicheza mpira wa pete katika Bonanza la Michezo kwa wafanyakazi wa Shirika hilo lililofanyika leo Septemba 17,2022 katika viwanja vya Chuo cha Ardhi Jijini Dar es Salaam.

Watumishi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) wakicheza mchezo wa kuvuta kamba katika Bonanza la Michezo kwa wafanyakazi wa Shirika hilo lililofanyika leo Septemba 17,2022 katika viwanja vya Chuo cha Ardhi Jijini Dar es Salaam.

********************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS), leo Septemba 17,2022 wameshiriki siku ya Bonanza la Michezo kwa wafanyakazi wa Shirika hilo dhumuni kuu likiwa nikuwakutanisha watumishi wa TBS katika michezo ili kuboresha afya na kujenga mahusiano mazuri miongoni mwa watumishi.

Akizungumza wakati wa Bonanza hilo lililofanyika Jijini Dar es Salaam, Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi TBS, Bw.Twalib Mmbaga amesema katika Bonanza hilo ambalo wameliita kwajina la 'Viwango Sports Bonanza'ni tukio linaloshindanisha watumishi wa shirika la viwango Tanzania katika michezo mbalimbali kama vile mpira wa miguu, mpira wa pete, mpira wa wavu, kuvuta kamba na michezo ya jadi ambapo mashindano hayo yanashindanishwa kiidara.

"Kupitia michezo hii watumishi wanapata burudani na kupunguza msongo wa mawazo unaoweza kutokana na kukosa nafasi ya kufanya mazoezi au kushiriki michezo mbalimbali". Amesema

Aidha amewapongeza wanaviwango waliojitokeza siku hiyo na walioona umuhimu wa kushiriki katika michezo hiyo ili kuboresha afya zao na kujenga mahusiano mazuri kati ya watumishi kwani utekelezaji mzuri wa majukumu ya kila siku hutegemea afya ya mwili na akili.

Pamoja na hayo ameipongeza menejimenti ya TBS kwa jitihada ilizozifanya kuweza kufanikisha Viwango Sports Bonanza kwani haikuwa rahisi ikizingatiwa kuwa shughuli kama hii inahitaji uwepo wa bajeti ili kufanikisha.

Share To:

emmanuel mbatilo

Post A Comment: