Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe (wapili kushoto) akizungumza jambo na Mkuu wa Kitengo cha Bima Benki ya CRDB, Moureen Majaliwa wakati wakitembelea mabanda katika tamasha la kutoa elimu ya bima kwa vyombo vya moto lililoandaliwa na Benki ya CRDB na kufanyika kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki. Wengine pichani ni Kaimu Mkurugenzi wa Wateja Wadogo na Wakati wa Benki ya CRDB, Bonaventure Paul (kulia) pamoja na Meneja Mwandamizi wa Mawasiliano na Mahusiano wa Benki ya CRDB, Emmanuel Kiondo.

========   ========  =======

Benki ya CRDB imezindua rasmi kampeni maalum ya elimu ya bima ya vyombo vya moto iliyopewa jina la ‘Kuwa Shua’ tamasha lililofanyika kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es salaam mwishoni mwa wiki.
 
Akizungumza katika tamasha hilo, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe alisema ili kuchochea ukuaji wa sekta ya bima na kuongeza ujumuishi wa sekta hii yaani “Insurance Inclusion,” Serikali kupitia Mpango Mkuu wa Maendeleo ya Sekta ya Fedha imekuwa ikiandaa programu mbalimbali za elimu kwa umma juu ya umuhimu wa matumizi ya bima.
 
"Ni imani yangu kuwa kampeni hii ya mwaka huu ya “Kuwa Shua” itawajengea uelewa wamiliki wa vyombo vya moto umuhimu wa kukata bima dhidi ya majanga yanayoweza kutokea, niipongeze Benki yetu ya CRDB kwa kutekeleza kwa vitendo agizo hili la ufikishaji wa elimu ya bima kwa wateja wenu na wananchi. Nafahamu mwaka jana mliendesha kampeni ya “Bima Unachokithamini” mkitoa elimu ya umuhimu wa bima katika nyanja mbalimbali". alisema Gondwe.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe (kulia) akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Maendeleo ya Biashara wa Kampuni ya Bima ya Sanlam, Ernest Selestine (watatu kushoto) wakati akitembelea mabanda katika tamasha la kutoa elimu ya bima kwa vyombo vya moto lililoandaliwa na Benki ya CRDB na kufanyika kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es salaam. Tamasha hilo liliwaleta pamoja wadau mbalimbali wa vyombo vya moto kama Kampuni za Bima, Mamlaka ya Usimamizi wa Bima (TIRA), Msuluhishi wa Migogoro ya Bima, Jeshi la Polisi, gereji pamoja na maduka ya vifaa mbalimbali za vyombo hivyo. Katikati ni Mkuu wa Kitengo cha Bima Benki ya CRDB, Moureen Majaliwa.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe (watatu kulia) akipata maelezo kutoka kwa Meneja Masoko wa Kampuni ya Bima ya Strategis, Lilian Malakasuka (katikati) wakati akitembelea mabanda katika tamasha la kutoa elimu ya bima kwa vyombo vya moto lililoandaliwa na Benki ya CRDB na kufanyika kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es salaam. Tamasha hilo liliwaleta pamoja wadau mbalimbali wa vyombo vya moto kama Kampuni za Bima, Mamlaka ya Usimamizi wa Bima (TIRA), Msuluhishi wa Migogoro ya Bima, Jeshi la Polisi, gereji pamoja na maduka ya vifaa mbalimbali za vyombo hivyo. Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Bima Benki ya CRDB, Moureen Majaliwa.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe akipata maelezo kutoka kwa Maafisa wa Shirika la Bima nchini wakati alipotembea banda lao katika tamasha la kutoa elimu ya bima kwa vyombo vya moto lililoandaliwa na Benki ya CRDB na kufanyika kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe furahi jambo na Maafisa wa Shirika la Bima la Zanzibar wakati alipotembea banda lao katika tamasha la kutoa elimu ya bima kwa vyombo vya moto lililoandaliwa na Benki ya CRDB na kufanyika kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es salaam.
 
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe akipata maelezo kutoka kwa Mdau mkuu wa ukarabari wa magari, Edwin Mactemba wakati alipotembea banda lake katika tamasha la kutoa elimu ya bima kwa vyombo vya moto lililoandaliwa na Benki ya CRDB na kufanyika kwenye viwanja vya Posta, Kijitonyama jijini Dar es salaam.





Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: