Mesoni Kashiro (15) Mkazi wa Kijiji Cha Gelailumbwa kata ya Gelailumbwa Tarafa ya Ketumbeine wilayani Longido Mkoani Arusha ameshambuliwa na mume wake Namendea Lesiria kwa kushirikiana na Rafiki yake ambaye jina halijafahamika kwa kosa la kumwaga dawa ya mfugo aina ya mbuzi.

"Huu ni ukatili kabisa kwanza ameolewa akiwa na umri mdogo ,wamempiga wakiwa wamemfunga kamba na kumtundika kwenye miti" alidai Chisunga

Hayo yameelezwa na Ofisa Ustawi wa Jamii wilayani hapa Atunagile Chisunga akieleza kuwa watuhumiwa wapo kituo Cha Polisi Longido na hapo kesho wanatarajia kufikishwa mahakamani huku akisistiza mama huyo yupo kituo Cha afya Longido akiendelea kupatiwa  matibabu zaidi.

Share To:

Post A Comment: