KARANI wa Sensa Kata ya Majimoto,  Halmashauri ya Wilaya ya Mpimbwe, mkoani Katavi, Kenan Kasekwa, amevamiwa usiku wa kuamkia leo na kuporwa kishikwambi cha kutunzia kumbukumbu za sensa.

Akithibitisha tukio hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Catherine Mashala, amesema karani huyo ambaye ni mwalimu, alivamiwa na mtu aliyevunja kitasa na kuingia chumbani, kisha kubeba kifaa hicho, fedha kiasi cha Sh 760,000, redio na vitu vingine.

“Inavyoonekana alipuliza dawa ya kuwalaza usingizi yeye na familia yake, yule mwizi aliingia chumbani akabeba ka lasketi, kishikwambi, fedha alizozikuta, simu na redio, “alisema Mashala.


Share To:

Post A Comment: