Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk. Binilith Mahenge akizungumza na Wananchi wa Kijiji cha Mughanga kilichopo Tarafa ya Mgori Wilaya ya Singida, kuhusu uharibifu unaofanyika katika Hifadhi ya Msitu wa Mgori waakati wa ziarayake ya siku moja ya kutembelea msitu huo ambapo aliambatana na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa na wilaya hiyo.
Dk. Mahenge akiangalia uharibifu wa msitu huo uliofanywa na wavamizi kwa kukata miti.
Mkuu wa Wilaya ya Singida, Paskas Mulagiri akizungumza wakati wa ziara hiyo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Eliya Digha akizungumza katika ziara hiyo.
Muhifadhi wa Misitu wa Wilaya ya Singida, Uswege Mwasumbi akitoa taarifa ya operesheni mbalimbali zilizofanyika za kuwaondoa wavamizi wa msitu huo.
Pikipiki yenye namba za usajili  T 869 CZR ikiwa na magunia ya mkaa baada ya mwendeshaji wake kukamatwa katika hifadhi hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Singida, Dk.Binilith Mahenge na Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wakijadiliana wakati wa ziara ya kukagua msitu huo.


Ziara hiyo ikifanyika.
Mifugo ikiwa ndani ya hifadhi hiyo.
Dk. Mahenge akiangalia wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama walivyokuwa wakibomoa moja ya nyumba isiyo rasmi iliyojengwa ndani ya hifadhi hiyo.
Ukaguzi wa msitu huo ukiendelea.
Wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wakiingia ndani ya nyumba isiyo rasmi iliyojengwa ndani ya hifadhi hiyo kabla ya kuibomoa.
Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wakiondoa gogo lililowekwa na wavamizi wa msitu huo kuzuia magari yasipite ili wasiweze kukamatwa.
Msafara wa magari ya wajumbe hao wakati wa ziarahiyo.
Baadhi ya wananchi wakiwa chini ya ulinzi wa polisi baada ya kukutwa ndani ya msibu huo. 
Diwani wa Kata ya Mughanga, Nassoro Hassan akizungumzia msitu huo mbele ya mkuu wa mkoa.
Mmoja wa wananchi wa kijiji hicho akielezea msitu huo na jinsi walivyo ondolewa kwenye hifadhi hiyo baada ya kulipishwa fedha ambapo alidai hawana sehemu ya kulima wala kujenga.

Ukaguzi wa msitu huo ukiendelea.


Na Dotto Mwaibale, Singida


MKUU wa Mkoa wa Singida, Dk. Binilith Mahenge amepiga marufuku wananchi kuingia ndani ya Hifadhi ya Msitu wa Mgori  kufanya shughuli za kilimo, kuchoma mkaa na kuchunga mifugo bila kibali kutoka kwa mamlaka zinazohusika na uhifadhi wa msitu huo uliopo Wilaya ya Singida.

Ametoa onyo hilo leo Julai 13, 2022 wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha  Mughanga baada ya Kamati ya Ulinzi na Usama ya Mkoa ilipotembelea msitu huo kujionea uharibifu uliofanywa na wavamizi huku wengine wakijenga nyumba za kuishi ndani ya hifadhi hiyo.

"Kwa sababu elimu tulikwishatoa na DC (Mkuu wa Wilaya) alipita vijiji vyote kutoa elimu ni marufuku kuingia ndani ya msitu huo na waambie yule mzee mwenye muvi (Dk.Mahenge) amekuja hana mzaha katika hili," alisema.

Dk.Mahenge alisema mtu yeyote atakayekutwa ndani ya msitu huo atakamatwa na kama ana mifugo nayo itakamatwa kutaifishwa na kuuzwa.

Alisema kuendelea kuharibu misitu ya hifadhi ni laana kubwa ambayo wajukuu zetu wataweza kuja kutuchapa tukiwa ahela.

"DC alipita Novemba 2021 na akatoa elimu watu wasiingie kwenye msitu,wasilime wala kufugia mifugo lakini cha kushangaza leo watu wameuvamia na wanagawana kama mashamba na wamejiwekea mipaka baada ya kugawana ekari zaidi ya 200 hadi 300 kwenye msitu huo wenye miti aina ya Mininga," alisema.

Mkuu wa Mkoa aliongeza kuwa baadhi ya maeneo wananchi wanahama na kwenda kuishi eneo jingine ili kupisha uhifadhi ili wanyama waendelee kuwepo na hivyo kuingizia serikali mapato ya fedha za kigeni kutokana na kutembelea hifadhi.

" Leo tunapata fedha kwasababu wazungu wanatoka kwao kuja kuangalia wanyama ambao kwao hawapo na sisi babu zetu waliwatunza wanyama ndio maana tumewakuta," alisema.

Dk.Mahenge aliwaomba wananchi kutoa ushirikiano kwa kuwafichua watu wanaohujumu msitu wa hifadhi wa Mgori ili hatua kali ziweze kuchukuliwa dhidi yao.

Awali Muhifadhi wa Misitu Wilaya ya Singida, Uswege Mwasumbi, alimweleza Mkuu wa Mkoa wa Singida kuwa nyumba  704 za wananchi waliovamia msitu huo ambao upo mpakani mwa Wilaya ya Singida Vijijini na Mkoa wa Manyara zimebomolewa wakati wa operesheni iliyofanywa na askari wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).

Mwasumbi alisema kati nyumba hizo zilizobomolewa 557 ni za ukanda wa eneo la kitongoji cha Kazamoyo ambalo ndilo lililoathirika zaidi na uharibifu wa ukataji miti ovyo kutokana na kuendesha shughuli za kilimo, ufugaji wa mifugo na uchomaji mkaa.

Alisema nyumba hizo zilibomolewa katika operesheni iliyofanyika mwezi Disemba mwaka jana ambapo eneo lililolengwa ilikuwa ni kitongoji cha Kazamoyo ambacho sio rasmi na hakitambuliwi na Serikali.

"Mifugo imebaki kuwa changamoto ndani msitu wa hifadhi Mgori na jeuri ya wafugaji ni kwamba wao wana nguvu ya pesa wanaweza kuwalaghai viongozi wa vijiji ili waendelee kuwepo ndani ya hifadhi hiyo," alisema.

Mkuu wa Wilaya ya Singida, Paskas Mulagiri, alisema kaya zaidi ya 200 ziliondolewa ndani ya hifadhi hiyo baada ya wananchi kuuziwa na viongozi wa Serikali za vijiji wasio waaminifu kwa kuwatoza fedha na kuwapa stakabadhi ambazo serikali ilikuja kubaini zilikuwa ni feki.

Mulagiri alisema baada ya kubaini hilo, serikali iliwachukulia hatua za kisheria viongozi wa Serikali za vijiji ambao walihusika na udanganyifu huo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Eliya Digha, alisema wavamizi wa msitu huo wengi wao sio wenyeji wa vijiji vinavyouzunguka bali wanatoka mikoa jirani.

 

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: