Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Mhandisi Kundo Mathew(Mb) amewataka wakazi

maeneo ya Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi kushiriki kikamilfu katika zoezi utekelezaji mfumo wa Anwani za Makazi 

pamoja na Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika mwezi Agosti 2022 


Mheshimiwa Mhandisi Kundo ameyasema hayo jana Alhamisi, Machi 10, 2022 Wilayani ya Bariadi Mkoa wa Simiyu

alipofanya ziara katika vijiji mbalimbali vya Wilayani humo ya kuhamasisha utekelezaji wa mfumo wa Anwani za Makazi

naotakiwa kukamiliza ifikapo mwezi Mei 2022.


Alisema kuwa wananchi wote wanaoshi katika Wilaya ya Bariadi wakashiriki kikamilifu katika 

utekelezaji mfumo wa Anwani za Makazi ili ukawe rahisi kwenda kutekeleza zoezi la 

Sensa ya watu na makazi litakalofanyika mwezi Agosti, 2022 ambalo litapelekea urahisi wa ufikishwaji wa huduma na

maendeleo kwa wananchi wa maeneo hayo kuendana na idadi yao


Nae Mkurugenzi wa Huduma za Posta wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Caroline Kanuti

alitumia fursa hiyo kuwaelezea wakazi wa Manisapaa ya Bariadi umuhimu wa mfumo wa Anwani za makazi  endapo 

watashiriki kikamilifu katika zoezi hilo.


“Pale ulipo unaweza ukapata tatizo, unauguliwa au nyumba imewaka moto au kuna mgonjwa anataka kupelekwa hospitali

unapiga simu unajitambulisha tu kwamba nipo kitongoji fulani unataja na namba ya nyumab yako kisha yule unaempigia

simu atakuja mapka pale ulipo kwahiyo kupitia mfumo wa Anwani za makazi inakuwa rahisi kupata msaada”.


Alisema kuwa mfumo wa Anwani za Makazi unarahisisha shughuli za mbalimbali ikiwemo za kilimo kwa

kununua mazao au pembejeo za kilimo popote ulipo na bidhaa yako kukufikia kwa urahisi.

Share To:

Post A Comment: