MKUU wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo  akiongeza na baadhi ya viongozi wa MBOMIPA pamoja na wadau wa jumuiya hiyo ya uhifadhi wa wanyama pori wilaya ya Iringa.
mwenyekiti wa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori katika Tarafa za Idodi na Pawaga (MBOMIPA) Jonas Mkusa akiongeza na baadhi ya viongozi wa MBOMIPA pamoja na wadau wa jumuiya hiyo ya uhifadhi wa wanyama pori wilaya ya Iringa.
Baadhi ya wajumbe wa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori katika Tarafa za Idodi na Pawaga (MBOMIPA) wakifuatilie semina ya uhifadhi wa wanyama pori wa jumuiya hiyo
Baadhi ya wadau wa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori katika Tarafa za Idodi na Pawaga (MBOMIPA) wakifuatilie semina ya uhifadhi wa wanyama pori wa jumuiya hiyo

Na Fredy mgunda,Iringa.

 

MKUU wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo ameutaka uongozi wa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori katika Tarafa za Idodi na Pawaga (Mbomipa) kuacha mara moja kutumia madaraka yao vibaya na kuwa chanzo cha migogoro baina ya jumuiya hiyo na wawekezaji.

Akizungumza wakati mafunzo kwa viongozi na wadau wa jumuiya hiyo,Moyo aliwataka viongozi hao kutafakari zababu zilizopelekea kufutwa kwa MBOMIPA miaka mitano iiliyopita na kuzifanyia kazi ili kuwa funzo la kukomesha migororo katika awamu hii.

Kiongozi huyo wa Wilaya ya Iringa alisema Serikali haiko tayari kushuhudia viongozi wa MBOMIPA wakitumia madaraka yao vibaya kwa kukwamisha mipango na maendeleo ya jumuiya hiyo wenye lengo la kuvutia wawezekezaji wengi zaidi katika maeneo ya hifadhi kwa manufaa ya wananchi wa vijiji 21.

Moyo alisema Serikali ya Wilaya ya Iringa inapenda kuona mabadiliko ya haraka katika kuimarisha uhai wa Jumuiya ya MBOMIPA, na Ufanisi chanya wa watendaji wa kila siku huku akihimiza ushirikiano baina ya wananchi wa vijiji vinavyonufaika, viongozi wa MBOMIPA na serikali ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

Alisema mafunzo wanayopatiwa viongozi na wadau wa Jumuiya hiyo ni mwanzo mzuri wa safari ya kuimarisha MBOMIPA mpya Kwani Wanahitajika wadau wa uhifadhi  ndani na nje ya nchi ili kuwezesha utaalam na Rasirimali fedha zitakazosaidia kuinua maendeleo ya wananchi.

Aidha Mkuu wa Wilaya Mohamed Hassan Moyo amewahimiza wadau wa Uhifadhi wa wanyama na Mazingira kuongeza jitihada za uhifadhi wa mazingira, misitu na vyanzo vya maji ambavyo utegemewa na watu, mifugo na wanyamapori hatua ambayo itasaidia kudhibiti athari za mabadiliko ya hali ya hewa na Tabia nchi.

“Tayari tumeanza kupata madhara makubwa katika maisha ya binaadam na pia kwa uchumi wa wananchi wetu na kuleta mzigo mzito kwa Taifa letu la Tanzania, Utafiti wa mabadiliko ya hali ya hewa na Tabia nchi umebaini ongezeko la hali ya joto pia ongezeko la tofauti la mienendo ya mvua na hasa upungufu wa rasilimali maji” Alisema Moyo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Jumuiya ya Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori katika Tarafa za Idodi na Pawaga (MBOMIPA) Jonas Mkusa alisema kuwa kusimama kwa shughuli za Jumuia hiyo kulikuwa na athari katika vijiji hasa kutokana na kukosa mapato yaliyokuwa yakipatikana awali kutokana na wadau walikuwa wamewekeza katika maeneo hayo

Mkusa alisema kurejea kwa jumuia hiyo ni jambo la faraja kwa wananchi wa vijiji 21 vinavyonufaika na MBOMIPA na kuhimiza ushirikiano utakaosaidia kuvutia wawekezaji na kuepuka kuzalisha migogoro isiyo na tija inayoweza kukwamisha maendeleo ya Jumuiya hiyo.

Mwenyekiti aliwahakikishia wananchi na wadau kuwa atahakikisha fursa zote zilizopo kupitia MBOMIPA zitakuwa wazi kwa ajili ya kufanikisha malengo yaliyokusudiwa huku akisisitiza kuwa uongozi wa Jumuiya hiyo hautokuwa kikwazo katika kufikia malengo.

 

Mbomipa ni Jumuiya inayoshughulika na uhifadhi wa Maeneo ya hifadhi ya wanyamapori ya jamii (WMA) nje ya mipaka ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha Wilayani Iringa, Wanyama walioko katika eneo hilo wanatoka ndani ya hifadhi hiyo na hifadhi ya mikumi.

Vijiji vinavyounda Jumuiya hiyo ni Idodi, Ilolompya, Isele, Kinyika, Kisanga,Luganga, Mafuluto,Magozi,Mahuninga, Makifu, Mboliboli, Mkombilenga, Nyamahana, Itunundu, Kimande, Malizanga, Mbuyuni, Mapogolo, Kitisi na magombwe.

 

Share To:

Post A Comment: