Picha ikimuonesha Bw. Abdala Taveli Mkulima kutoka skimu ya kilimo cha umwagiliaji ya Kiwere Inayotumia Teknolojia ya kinyonga, wilayani Iringa |
Mhandisi wa Umwagiliaji Mkoa wa Iringa Onesmo Kahogo alipokuwa akizungumza kuhusu teknolojia ya kilimo cha umwagiliaji maarufu kwa jina la Kinyonga. |
Wakulima katika skimu za kilimo cha
umwagiliaji Kiwere na Mafuruto, wamenufaika na teknolojia ya kisasa katika
setka ya kilimo cha Umwagiliaji, ambayo ni mbadala wa matumizi ya rasimali
maji,maarufu kwa jina la kinyonga.
Mhandisi wa Umwagiliaji mkoani Iringa Onesmo Kahogo, amesema
mwishoni mwa wiki mkoani Iringa kua, teknolojia hii inasaidia kukabiliana na
athari zitokanazo na mabadiliko ya Tabianchi, kwani itamsaidia mkulima kupima
kiwango cha maji anayohitaji kutimia shambani na haina madhara kwa mazao.
Mhandisi Kahogo alisema Teknolojia hii imesaidia kupungua
migogoro ya maji kwa wakulima na inampa
mkulima nafasi ya kufanya shughuli nyingine za uzalishaji.
Teknolojia hiyo inayotumia kifaa maalum kinachofukiwa
nardhini ambacho, kinaruhusu eneo linalotumika kwa kilimo wa wakati huo kutumia
maji yanayotosha kumwagiliwa katika eneo husika na kwa kiasi ambacho mkulima
anakuwa amejipimia kulingana na mahitaji ya maji kwa wakati huo.
Kwa upande wake katibu wa skimu ya Kiwere maarufu kwa jina la
tupendane Bw. Abdalah Taveli, amesema teknolojia hiyo inasaidia kupata mazao
mengi kwa kutumia maji kidogo akitolea mfano ya mavuno ya gunia sabini za
vitunguu katika hekari moja.
Alisema kuwa pamoja na teknolojia hiyo kutumia maji kidogo
inasaidia pia matumizi madogo ya pembejeo, kutokana na kwamba hazisombwi na
maji shambani.
Post A Comment: