Na Rhoda Simba,Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Antony Mtaka ameuagiza uongozi wa Ofisi ya Mkurugenzi wa jiji na Afisa Elimu kuhakikisha  wanasambaza walimu wa sekondari katika shule zenye uhaba badala ya kuacha walimu kurundikana shule moja.


Aidha amesema zipo shule za sekondari ndani ya jiji ambazo zina walimu  wengi na zilizopo  pembezoni mwa jiji zina walimu wachache, kutokana na hali hiyo Ofisi ya afisa elimu na Ofisi ya Mkurugenzi wa jiji waone namna ya  kuweza kuwasambaza walimu waliokuwa wengi katika shule za  pembezoni ambazo zina uhaba.

 

Mtaka ameyasema hayo leo Disemba 22 jijini hapa wakati wa ziara ya ukaguzi wa ujenzi  wa vyumba vya madarasa katika shule za sekondari zilizojengwa kwa fedha za mkopo wa mashart nafuu unaotokana  na mapambano dhidi ya uviko 19.


Amesema Mkoa  wa Dodoma ni kati ya mikoa ambayo imefanikiwa kufanya ujenzi wa vyumba bora  vya madarasa ambayo yana ubora wa kiwango cha juu


"Dodoma tumeweza kujenga madarasa yenye ubora unaoendana na thamani ya fedha lakini napenda kutoa maagizo katika Ofisi  ya Mkurugenzi na afisa elimu kukutana mkaona ni namna gani ya kufanya utaratibu wa kupunguza 

 walimu  waliozidi katika baadhi ya shule na kuwapeleka katika shule ambazo zina uhaba wa walimu,


"Na jambo hili liwekwe wazi kwa walimu kuwa ni kwa nia njema ili kuifanya  elimu ya wanafunzi wa jiji la Dodoma kuwa bora  zaidi na ilingane na viwango vya ubora wa madarasa" amesema Mtaka


Hata hivyo ametoa maelekezo kwa Ofisi ya Mkurugenzi wa jiji la Dodoma na Ofisi ya afisa elimu wa jiji kutoa  taarifa kwa wakuu wote wa shule  kuwa pindi shule zitakapofunguliwa  tarehe 17 January 2022 kila mwanafunzi awajibike kupanda miti na kuuutunza.


Nae Mkurugenzi wa jiji Joseph Mafuru amesema ujenzi huo unatarajia kabla ya sikukuu ya chris mass utakuwa umekamilka na funguo zitakabidhiwa tayari kwaajili ya  maandalizi  ya wanafunzi kuanza masomo.

Share To:

Post A Comment: