Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Naghenjwa Kaboyoka akiwapongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa matumizi mazuri ya fedha za Serikali katika kutekeleza miradi ya usambaji umeme wilayani Manyoni mkoani Singida baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo leo. Kushoto ni Makamu .wa kamati hiyo, Japhet Hasunga na kulia ni Waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani.


Waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani, akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo.

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Rahab Mwagisa, akizungumza kabla ya kuanza kikao hicho. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya REA,, Wakili Julius Bundala. 


Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Naghenjwa Kaboyoka, akizungumza na wananchi wa eneo la Majengo baada ya kuikagua Shule ya Sekondari ya Mlelwa iliyopata umeme wa REA.
Moja ya jengo la  Shule ya Sekondari ya Mlelwa iliyopata umeme wa REA.
Baadhi ya Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na REA wakiwa kwenye kikao hicho.

Kikao kikiendelea.
Kikao kikiendelea.
Wajumbe wa kamati hiyo wakisikiliza kwa makini taarifa ya mradi huo. Kulia ni Mhandisi Isack Kamwelwe na kushoto ni Hamis Kigwangala.

Baadhi ya Watumishi  wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na REA wakiwa kwenye kikao hicho.



Oparesheni Meneja wa Kiwanda cha kuchakata mafuta ya alizeti cha Qstek, Elifadhil Ezekiel (kulia), akitoa maelezo mbele ya kamati hiyo ilipotembelea kiwanda hicho
Muonekano wa kiwanda hicho kilichopata umeme wa REA.

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mlelwa, Elias Deogratius, akizungumzia mafanikio wanayopata baada ya kuwekewa umeme wa REA.


Baadhi ya wananchi wa eneo la  Majengo na wajumbe wa kamati hiyo wakiwa kwenye mkutano baada ya kamati hiyo ya PAC kutembelea  Shule ya Sekondari ya Mlelwa.

Mkazi wa Majengo John Joshua akiishukuru Serikali na REA kwa kuwapelekea umeme.

Juma Amran akiipongeza REA kwa kupeleka umeme katika Shule ya Sekondari ya Mlelwa.




Fundi Sanifu wa Halmashauri ya Mji Mdogo wa Wilaya ya Itigi, Godfrey Byamungu, (kushoto) akitoa taarifa kwa kamati hiyo kuhusu mradi wa maji wa Kisima  kilichopo eneo la Raundi  Abauti mjini humo.

Wajumbe wa kamati hiyo wakisilika kwa makini taarifa ya mradi huo. 




Na Dotto Mwaibale, Manyoni


MWENYEKITI wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Naghenjwa Kaboyoka amewapongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa matumizi mazuri ya fedha za Serikali katika kutekeleza miradi ya usambaji umeme wilayani Manyoni mkoani Singida.

Kaboyoka ametoa pongezi hizo kwa nyakati tofauti leo  wakati kamati hiyo ilipokuwa ikitembelea miradi ambayo imetekelezwa na REA katika wilaya hiyo.

Miradi iliyotembelewa  na kukaguliwa ni uwekaji wa umeme katika Kiwanda cha Qstek ambacho kitakuwa kikichakata mafuta ya alizeti, Shule ya Sekondari ya Mlelwa na Kisima cha maji kilichopo eneo la Raundi  Abauti Itigi mkoani humo.

" Tumekuja kutembelea miradi hii ili tujiridhishe kwa macho na kuona uhalisia wa fedha zinazotolewa na Serikali kama zinatumika ipasavyo tunawapongeza REA kwa kazi  nzuri mliyoifanya." alisema Kaboyoka.

Waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani akitoa taarifa mbele ya kamati hiyo alisema wizara hiyo kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kuwezesha utekelezaji wa miradi ya nishati vijiji katika maeneo mbalimbali nchini ikiwemo Mkoa wa Singida.

" Mradi unaotekelezwa kwa sasa mkoani Singida ni mradi wa kusambaza umeme vijijini Awamu ya Tatu Mzunguko wa Kwanza." alisema Kalemani.

Dkt. Kalemani alisema lengo la Serikali ni kuhakikisha kila kitongoji hapa nchini kinapata umeme ambapo ametoa wito kwa wananchi kuingiza umeme katika nyumba zao kwa bei ya Sh.27,000 tu hata kama wanaziona mbaya ili mradi wawe wanaishi humo.

"Niwaombe watanzania kila penye mradi wa wananchi unaohitaji umeme waweke nishati hiyo kwani itawapunguzia gharama ya kuiendesha na kuwa suala la wananchi kupata umeme ni la lazima." alisema Kalemani.

Mkazi wa Majengo wilayani humo, John Joshua aliishukuru Serikali na REA kwa kuwapelekea umeme lakini akaomba changamoto ya kukosekana kwa nguzo iangaliwe.

Juma Amran aliipongeza REA kwa kupeleka umeme katika Shule ya Sekondari ya Mlelwa na akaomba wasaidiwe kupata maji kwani hiyo ndiyo changamoto yao kubwa.

Mkuu wa shule hiyo ya Sekondari ya Mlelwa, Elias Deogratius alisema baada ya kuwekewa umeme ufaulu wa wanafunzi umeongezeka kwa kiasi kikubwa kutokana na kupata muda wa kutosha wa kujisomea vizuri.

Share To:

Post A Comment: