Rais Magufuli aliyekuwa mapumzikoni nyumbani kwake, Chato mkoani Geita amewasili jana Alhamisi Januari 9, 2020 jijini Dar es Salaam.

Mara baada ya kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam akiwa na mkewe, Janeth, Rais Magufuli alisalimiana na baadhi ya wafanyakazi katika uwanja huo.

Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais- Ikulu ya Tanzania, Gerson Msigwa amesema leo  Ijumaa Januari 10, 2020 Rais Magufuli ataanza ziara ya kikazi ya siku tano visiwani Zanzibar.
Share To:

Post A Comment: