Na Ferdinand Shayo,Arusha.
Maelfu ya Watanzania wamefanya maombi
ya kumuombea Raisi wa Tanzania Dr.John Pombe Magufuli pamoja na Viongozi wa
serikali ili kuendeleza nguvu katika ujenzi wa Tanzania mpya ili kufukia uchumi
wa Viwanda kama ilivyo ndoto ya Raisi.
Mji wa Arusha umefurika maelfu ya watu
kutoka ndani na nje ya mkoa wa Arusha pamoja na mikoa ya
Kilimanjaro,Manyara,Singida, Dodoma ambao wamekusanyika kwa ajili ya kuiombea
serikali na Watanzania kwa ujumla.
Mkurugenzi Msaidizi wa Redio Safina
,Hellen Lema amesema kuwa maombi hayo yanalenga kuomba Mungu azidi kumpa nguvu
Raisi Magufuli ili aweze kuwatumikia vyema Watanzania na taifa la Tanzania lizidi kubarikiwa na
kusonga mbele kiuchumi.
Mchungaji Pascal Thomas amesema kuwa maombi hayo ya toba dhidi ya maovu mbalimbali na kuhamasisha watu
kumcha Mungu na kuondokana na uovu pamoja na kuwaombea viongozi.
Kwa upande wao wananchi Ester Mremi na Joel Molel walioshiriki katika maombi hayo
wameeleza umuhimu wa kuliombea taifa ili kuwa na muelelkeo chanya wa
kimaendeleo na kufungua milango ya kiuchumi ili waweze kufanikiwa.
Post A Comment: