Kijana mmoja aliyetambulika kwa jina moja la Boniface mkazi wa Mwananyamala kwa Msisiri anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni kwa tuhuma za kuiba masanduku ya kuzikia (majeneza) mawili na kuyaficha nyuma ya choo cha mkazi mwingine wa mtaa huo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Jumanne Muliro, amesema tukio hilo limetokea kati ya ofisi mbili za kuuza masanduku hayo ambapo moja ndiyo iliyoibiwa majeneza hayo. Amesema jeneza moja ni la mtu mzima na moja likiwa la mtoto mdogo

“Kuna work shop mbili ambazo zinajishusisha na kutengeneza masanduku, zipo kwenye sehemu moja, asubuhi mtu kaingia kwenye work shop yake akakuta masanduku mawili hayapo akaanza kufuatilia, baada ya muda akajua yapo kwenye workshop nyingine, kwa hiyo kilichofanyika ni ufuatiliaji na askari wakafanikiwa kuyapata, ni suala ambalo linachunguzwa kujua kama wanadaiana au ni wizi umefanyika, ndipo sheria ifuate”, amesema Kamanda Muliro.

Mmiliki wa masanduku hayo Bi. Judith Carlos amesema masanduku hayo aligundua yapo kwa jirani yake baada ya kumuahidi mtu atampa elfu 50 iwapo atamsaidia kujua nani kayachukua, na ndipo baadaye akaambiwa mahali yalipo.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: