6945
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akiwaeleza watumishi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) umuhimu wa kubeba  ajenda ya ujenzi wa uchumi wa Viwanda wakati wa ziara yakutembelea vyombo vya habari Mkoani Dodoma  iliyoanza mapema leo.
6994
Muwakilishi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali Mkoani Dodoma Bw.Felix Mushi akisisitiza jambo wakati wa ziara ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi katika Ofisi za Kampuni hiyo Mkoani Dodoma.
7054
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi  akiwa kwenye picha ya pamoja na watumishi wa Kampuni ya                         Magazeti ya Serikali (TSN) Mkoa wa Dodoma mara baada ya kutembelea Ofisi hizo mapema leo ili kujionea utendaji wa Kampuni hiyo na Kusisitiza uzingatiaji wa maadili ya uandishi  wa habari.
7065
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali Dkt. Hassan Abbasi akiagana na watumishi wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Mkoani Dodoma mara baada ya ziara yake katika Ofisi za Kampuni hiyo mapema leo.
7118
7120
………………….
Na Beatrice Lyimo-MAELEZO, DODOMA
Mkurugenzi wa Idara Habari( MAELEZO) Dkt. Hassan Abbasi ameanza ziara ya kutembelea vyombo vya habari Mkoani Dodoma kwa lengo la kuona na kujua changamoto za kiutendaji pamoja na jinsi gani wamejipanga juu ya Serikali kuhamia Dodoma.
Akiwa katika Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Dkt. Abbasi amevitaka vyombo vya habari vya Dodoma kuwa tayari na ujio wa Serikali kuhamia Dodona kwani matukio mengi ya kiserikali yatafanyika Mkoani humo.
“Kwa baadhi ya matukio yaliyofanyika hapa Dodoma nimeona uzubaifu kwa baadhi ya waandishi wa habari hivyo wanahabari wenzangu tuchangamke kwani matukio mengi ya Serikali yatafanyika hapa” amefafanua Dkt. Abbasi.
Aidha, Dkt. Abbasi ameutaka uongozi wa TSN kufuata maadili katika utendaji kazi kwani wananchi hutazama kampuni hiyo kwa jicho la utofauti kama chombo cha Serikali.
“Mkiwa kama Kampuni ya Magazeti ya Serikali mnatakiwa kuibeba agenda kuu ya Serikali ya Awamu ya Tano kufikia uchumi wa kati kupitia Viwanda” ameongeza Dkt.Abbasi.
Akiwa katika Ofisi za Mwananchi Communications Ltd mkoani humo, Dkt Abbasi amesema kuwa asilimia 99 ya waandishi wamejikita katika masuala ya kisiasa kuliko masuala ya maendeleo ya nchi au bajeti mbalimbali zinazohusu serikali hivyo ameshauri vyombo vya habari kujikita katika zaidi katika masuala ya maendeleo kwa manufaa ya jamii.
Aidha, Dkt. Abbasi amesisitiza umuhimu wa wanataaluma ya habari kujiendeleza kitaaluma ambapo kwa mujibu wa Sheria ya Huduma za Habari, mwandishi wa habari atatakiwa kuwa na  atashahada ya taaluma ya uandishi wa habari.
Akizungumzia kuhusu upatkanaji wa habari, Dkt. Abbasi amesema kuwa Serikali imewekeka mfumo wa kisheria kurahisisha upatikanaji wa taarifa mbalimbali kutoka katika Wizara na Taasisi zake.
Mbali na hayo Dkt. Abbasi amesisitiza waandishi wa habari kujisajili ili wapatiwe vitambulisho (Press Card) kwani kuanzia mwezi Machi mwaka huu katika matukio yote ya viongozi wakuu wa Kitaifa,  kila mwanahabari atatakiwa kuwa na kitambulisho hicho.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: