Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza majina ya wanachama wake walipitishwa kugombea ubunge wa Kinondoni na Siha Februari 17.

Taarifa ya Mkurugenzi wa Itikadi, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa Chadema, John Mrema aliyoitoa leo Januari 19, 2019 amesema walipitishwa ni Elvis Christopher Mosi kugombea Siha na Salimu Mwalimu kugombea Kinondoni.

“Kamati Kuu ya Chama imemaliza vikao vyake leo Januari 19, 2018 na imefanya uamuzi wa kushiriki kwenye uchaguzi mdogo kwenye majimbo ya Kinondoni na Siha unaotarajiwa kufanyika Februari 17, 2018,” amesema Mrema na kuongeza,

“Wagombea wote wameshachukua fomu za uteuzi kutoka kwa  wasimamizi wa uchaguzi kwenye majimbo husika na watazirejesha kesho Jumamosi Januari 20,  2018 , kwa ajili ya uteuzi.”
Share To:

msumbanews

Post A Comment: