Siku hiyo siwezi kuisahau, hata kama nitazeeka. Ilikuwa ni siku ya Jumamosi, majira ya saa mbili asubuhi, niliporudi nyumbani mapema kutoka sokoni baada ya kusahau mkoba wangu. Nilipoingia chumbani kwangu, sikutegemea kabisa kuona kile nilichokiona.
Mume wangu aliyekuwa ameniahidi uaminifu wa milele, alikuwa kitandani na bosi wangu wa kazi mwanamke ambaye nilimwamini sana, ambaye alikuwa kama dada yangu mkubwa.
Nilishtuka, nikakosa hata nguvu ya kuhema. Waliposhtuka kuniangalia, waliruka kitandani na kuanza kutoa visingizio visivyokuwa na kichwa wala miguu.
Nilihisi kama dunia imeanguka juu yangu. Machozi yalinibubujika kwa uchungu na hasira. Niliwageukia na kusema kwa sauti ya chini lakini yenye uzito, “Mmeharibu kila kitu.” Baada ya tukio hilo, maisha yangu yalibadilika. Nilikuwa na hasira, huzuni, na chuki ndani yangu. Kazini sikuweza tena kustahimili kumuona bosi wangu, hivyo nikaandika barua ya kuacha kazi.
Nyumbani hali ilikuwa mbaya zaidi mume wangu alianza kujitetea kwa kunilaumu eti nilikuwa nikimnyima haki zake za ndoa. Alisema nilikuwa mbali kihisia, na kuwa hiyo ndiyo sababu ya yeye kutafuta “faraja” kwingine.
Nikiwa nimevurugika kiakili na kihisia, rafiki yangu wa karibu alinitembelea na kunikuta katika hali ya unyonge mkubwa.SOMA ZAIDI.
Post A Comment: