Kwa zaidi ya miezi mitatu, usingizi haukuwahi kuwa wa amani katika familia yetu. Kila usiku, hasa saa sita kamili, mtoto wetu mchanga alikuwa akiamka kwa vilio vya ajabu, vilivyokuwa na sauti ya hofu, maumivu, na mshtuko.

Mwanzo tulidhani ni ndoto za kawaida au labda tatizo la kiafya la mtoto, lakini tulipojaribu kumpeleka hospitali, madaktari hawakugundua tatizo lolote.

Kila mara alipoamka kwa vilio hivyo, hakuwa na homa, hakulalamika maumivu ya tumbo, na mara nyingi alitulizwa haraka lakini baada ya dakika chache, kilio kilianza tena. 

Kama mzazi, ni jambo la kutisha kuona mtoto wako akiteseka na huwezi kuelewa sababu. Nilianza kuchunguza mazingira ya chumba chetu. Nikahakikisha hakuna mbu, baridi kali wala kelele za usiku zinazoweza kumsumbua.

Lakini hakuna kilichobadilika. Tulijaribu kulala chumba kingine kwa wiki moja, na cha kushangaza mtoto alilala kwa utulivu kabisa. 

Lakini mara tu tuliporudi kwenye chumba chetu cha kawaida, vilio vilirejea saa hiyo hiyo saa sita usiku. Siku moja, nikiwa nimemchukua mtoto chumbani kumtuliza, nilihisi baridi kali ikipita miguuni mwangu kana kwamba mtu alikuwa amepita. SOMA ZAIDI.
Share To:

Post A Comment: