Katika maisha ya kila siku, changamoto za kibiashara kwa wafanyabiashara wadogo mara nyingi ni kubwa kuliko faida wanayopata, na hii huwafanya wengi kuishi maisha ya msongo wa mawazo bila kuona matumaini mbele yao, kwani hasara ndogo ya kila siku huongezeka na kuwa mzigo mkubwa unaosababisha kukata tamaa.

Wafanyabiashara wadogo kama wale wa sokoni, wenye vibanda vidogo vya kuuza bidhaa au hata wale wanaouza mitaani hukumbana na changamoto za ushindani, mfumuko wa bei na wateja wasio na uaminifu, jambo linalowafanya wengi kuishi maisha ya kupambana kila siku bila kuona mwanga wa mafanikio.

Ni hali ya kawaida kwa mfanyabiashara mdogo kutumia mtaji wake wa mwisho kuagiza bidhaa, kisha ghafla akashangaa bidhaa hizo kutoleta faida, au pesa yake kumezwa na madeni yasiyolipika kutoka kwa wateja waliomuamini. Hali kama hiyo hupelekea msongo wa akili, kufilisika na hata kuvunjika kwa familia kutokana na ugumu wa maisha. Soma zaidi hapa 

Share To:

contentproducer

Post A Comment: