Kwa miaka minne ya ndoa yangu, nilikuwa kama mgeni ndani ya nyumba yangu mwenyewe. Mume wangu alikuwa tajiri wa kutupwa anaendesha biashara kadhaa jijini Mwanza, anamiliki magari ya kifahari na hata nyumba kadhaa.

Lakini pamoja na utajiri wake wote, hajawahi kunipa hata shilingi mia moja kwa hiari. Kila mara nilipohitaji hela ya matumizi au hela ya kwenda saluni, ilikuwa lazima niombe kwa unyenyekevu hadi nahisi kama ombaomba. Hata nguo zangu nyingi zilinunuliwa na dada zangu au marafiki walionionea huruma.

Kwa nje tulionekana familia ya kupendeza. Tulivalia vizuri, tuliishi kwenye nyumba nzuri, lakini ndani ya moyo wangu kulikuwa na kilio kisicho na sauti. Nilishindwa kuelewa kwa nini mume tajiri kabisa anaweza kuwa na roho ngumu kiasi cha kuniangalia nikihangaika, wakati pesa iko mezani kwake.

Nilijaribu kila njia kumvutia: kumpikia vizuri, kumjali, kumpa heshima, hata kumletea zawadi ndogo ndogo. Lakini moyo wake ulionekana kuwa na barafu badala ya upendo. Alikua mpole lakini mkavu hakuwa katili, lakini hakuwa pia mtu wa kuonyesha mapenzi au ukarimu. Soma zaidi hapa 

Share To:

contentproducer

Post A Comment: