Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Mhe. Ummy Nderiananga, ameshiriki mkutano wa dharura wa Kamati ya Mawaziri wanaohusika na Usimamizi wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa SADC, uliofanyika leo tarehe 13 Mei 2025 kwa njia ya mtandao.
Mkutano huo wa dharura umelenga kujadili hatua za kuimarisha mfumo wa usimamizi wa maafa na huduma za kibinadamu kwa nchi wanachama wa SADC.
Pia Mkutano huo umelenga kujadili hatua za kuimarisha usimamizi wa maafa na kuunga mkono ushirikiano wa kikanda katika kukabiliana na maafa na kuendelea kujenga usalama wa watu na mali, Aidha Waziri wa Serikali za Mitaa na Kazi za Umma wa Zimbabwe, Bw. Daniel Garwe, ameongoza mkutano huo kama Mwenyekiti.
Pamoja na hayo Mhe. Ummy Nderiananga ameutumia mkutano huo kutoa pongezi kwa Sekretarieti ya SADC kwa kuanzisha kituo cha huduma za kibinadamu na operesheni za dharura kilichopo Msumbiji, akisisitiza umuhimu wa kituo hicho katika kuimarisha ushirikiano na kukabiliana na maafa. Pia, amekubaliana na ongezeko la wataalamu 35 katika timu ya SADC ya utayari wa kukabiliana na dharura.
Mkutano huu umeonesha mshikamano wa kikanda katika kuimarisha usalama na kukuza uchumi wa nchi za SADC kupitia usimamizi bora wa maafa.
Post A Comment: