1....jpeg
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Elimu ya Afya kwa Umma kutoka Wizara ya Afya Dkt. Ona Machangu akiwa katika picha ya pamoja na Washiriki wa Mafunzo ya HCD Halmashauri ya Ushetu Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.
2.jpeg
3.jpeg

Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Elimu ya Afya kwa Umma kutoka Wizara ya Afya Dkt. Ona Machangu akizungumza kwenye  Mafunzo ya HCD Halmashauri ya Ushetu Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

3....jpegHCD_24.jpg

Kaimu Meneja Mpango wa Taifa wa Chanjo kutoka Wizara ya Afya Lotalis Gadau akizungumza kwenye  Mafunzo ya HCD Halmashauri ya Ushetu Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

HCD_3.jpg
Mratibu wa Mafunzo ya HCD Simon Nzilibili kutoka Wizara ya Afya  akizungumza kwenye  Mafunzo hayo  Halmashauri ya Ushetu Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.
HCD_32.jpg
Baba Kinara wa Uelimishaji kuhusu umuhimu wa huduma za Chanjo, Ammad Issa  akizungumza kwenye  Mafunzo hayo  Halmashauri ya Ushetu Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.




Na.Elimu ya Afya kwa Umma.


Imeelezwa kuwa huduma za chanjo husaidia kwa kiwango kikubwa katika kinga kwenye ukuaji wa mtoto hata mtu mzima na kuepuka magonjwa yanayozuilika kwa chanjo na kuokoa maisha.

 

Hayo  yamebainishwa    na Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Elimu ya Afya kwa Umma kutoka Wizara ya Afya Dkt. Ona Machangu   kwenye Mafunzo ya HCD yanayolenga kushirikisha jamii kwa kutumia mbinu Bunifu na Shirikishi  katika kutatua changamoto zinazopelekea jamii kuwa na mtazamo hasi kuhusu umuhimu wa huduma za  chanjo yanayofanyika katika Halmashauri ya Ushetu Wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

 

Aidha, Dkt. Ona ametoa rai kwa wakazi wa Ushetu na Tanzania kwa ujumla kuweka kipaumbele huduma za chanjo hivyo kupitia mafunzo ya “HCD”yatasaidia kuongeza wigo huduma za chanjo.

 

“Chanjo ina umuhimu mkubwa kwa binadamu hususan kuanzia mtoto mdogo ,mimi mwenyewe mnufaika wa chanjo, kwa hiyo nitoe rai kwa  wananchi wa Ushetu kuona umuhimu wa watoto wao kuwapeleka kupata huduma za chanjo kwani chnjo ili mtoto asipate maambukizi mfano Polio, Surua na magonjwa mengine yanayozuilika kwa chanjo ”amesema.

 

Halikadhalika, Dkt. Machangu amesema Wizara ya Afya imeendelea kutoa elimu ya afya kuhusu huduma za chanjo kwa kushirikiana makundi mbalimbali ya kijamii kupitia Mafunzo ya Human Centered Design-HCD ikiwemo makundi ya viongozi wa dini,Tiba Asili, Viongozi wa  Sungusungu, pamoja na vipeperushi na umuhimu wa matumizi ya namba 199 kwa ajili ya taarifa sahihi za elimu ya afya.

 

Akizungumzia madhara ya mtoto  endapo hatopata chanjo,Kaimu Meneja wa Mpango wa Taifa wa Chanjo  kutoka Wizara ya Afya Lotalis Gadau amesema kunaweza kusababisha ulemavu wa kudumu ikiwemo kutoona, kupooza au kupoteza maisha.

 

“Mtoto asipopata chanjo inaweza kupelekea ulemavu wa kudumu, mfano kupooza au upofu  au kupoteza maisha”amesema Gadau.

 

Pia, Gadau amesema ukosefu wa chanjo unaweza kusababisha changamoto ya Saratani ya Mlango wa Kizazi kwa Wanawake,hivyo ni muhimu wasichana kupata chanjo hiyo muhimu.

 

 Kwa upande wake Baba Kinara wa Uelimishaji kuhusu umuhimu wa huduma za Chanjo, Ammad Issa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wasioona Manispaa ya Tabora amesema alizaliwa mzima baada ya miaka miwili ulitokea ugonjwa wa Surua lakini alichelewa kupata matibabu hali iliyopelekea kuwa na ulemavu wa kudumu wa kutoona huku akitoa wito kwa wazazi kuacha mila potofu kuhusu chanjo.


“Nilizaliwa nikiwa mzima baada ya kufikisha miaka miwili ulitokea ugonjwa wa Surua wazazi wangu wakanipeleka kwa waganga wa Tiba Asili wakifikiri kuwa nimelogwa na hii ilitokana na mimi kukosa chanjo ya Surua, na enzi hizo walifikiri kila ugonjwa umelogwa hivyo nilitafutiwa dawa na kufukizwa na kunyweshwa dawa za kienyeji  na baadaye wakanipeleka hospitalini kwa kuchelewa na bahati mbaya nikawa kipofu hadi leo na niwasihi ndugu zangu chanjo zote ni muhimu mimi nilikosa chanjo na sioni mpaka leo hii ”amesisitiza .

..

 

Ikumbukwe kuwa Mafunzo ya HCD  ni mfumo  bunifu inayoshirikisha jamii moja kwa moja hadi hatua za mwisho kutatua changamoto katika jamii  ili kuwa na uelewa wa pamoja kwenye utatuzi wa changamoto hiyo.

Share To:

Post A Comment: