Na Denis Chambi, Tanga.


KUELEKEA uchaguzi wa viongozi wa Serikali za mitaa  wa mwaka 2024 na ule wa madiwani, wabunge na Rais  utakaofanyika mwaka  2025 mbunge   wa viti maalum mkoa wa Tanga Husna Sekiboko amewataka  umoja wa wanawake wa chama cha Mapinduzi 'CCM' kutumia vyema  falsafa nne '4R' za Rais  Dkt. Samia Suluhu Hassan kuanzia mchakato wa uchaguzi ndani ya Chama hicho

Falsafa hizo ambazo ni  Reconciliation (Maridhiano) ,Resilience (Ustahimilivu) , Reform (Mabadiliko) na Rebuild (Kujenga upya) amesema zikitekelezwa vyema  zitawezeaha kuzidi kukiimarisha chama hicho kuelekea chaguzi zote zitakazofanyika..

Sekiboko ametoa wito wakati wa mkutano wa Baraza wa wajumbe wa mkutano mkuu wa umoja wa wanawake  'UWT' mkoa wa Tanga ulioongozwa na Mwenyekiti wake  Alshaymaa Kwegyir ambapo ametoa simu  janja  10 kwa Kila jumuiya zenye thamani ya shilingi Milion12 katika wilaya zote 9 za mkoa huo zitakazotumika kwaajili ya kusajili wanachama wapya kwa njia ya kielektroniki ili kuongeza idadi yao na kuwawezesha kushinda kwenye chaguzi zote kuanzia ngazi ya vijiji, vitongoji na mitaa.

"Mwenyekiti wetu wa chama Cha Mapinduzi Taifa Dkt Samia Suluhi Hassan ameweka mkazo sana katika kutumia zile 4R zake nne anataka twende kwa wananchi tuwaelimishe na wakipende chama chetu, tuwasajili watambulikane kwenye chama chetu na mwisho wa siku tupate ushindi wa Kishindo ambao Rais wetu anautamani" alisema

Mbunge huyo amewasisitiza makatibu wa wilaya zote za mkoa wa Tanga  kwenda kutumia vyema nafasi zao kuhakikisha wanaongeza idadi ya wanachama  wapya ambapo mpaka kufikia sasa jumuia ya umoja wa wanawake  'UWT' imefikisha wanachama zaidi ya 9052  huku lengo likiwa ni kupata wanachama laki tatu kwa mwaka. 

"Sasa katika kutekeleza maelekezo ya Rais na Mwenyekiti wetu wa Chama Cha Mapinduzi Taifa   nilileta simu kwaajili ya usajili wa wanachama  ndani ya jumuia ya wazazi, vijana na UWT nimewiwa  kwasababu tunakwenda kwenye uchaguzi na shauku ya chama chetu ni kuwa na wanachama  wengi kuelekea chaguzi zote mbili naamini  kupitia jumuia zetu zote ushindi wa chama chetu utapatikana kwa kishindo" alisema  Mbunge huyo. 

"Kwa sababu shauku ya chama chetu ni kupata mtaji wa wanachama wengi ili kujihakikishia mtaji wa wapiga kura  mwaka huu na mwakani naamini ushindi wa chama Cha Mapinduzi  ndio utakaonipa uhakika wa mimi kurudi 2025  mshikamano katika jumuia hizi, mashirikiano  umoja wetu  utahakikisha kwamba tunampatia kura za kutosha Dkt Samia Suluhi Hassan  kupigiwa kura kwa mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu"

Kaimu katibu  wa umoja wa wazazi mkoa wa Tanga Urassa Kanyaro  amempongeza na kumshukuru mbunge wa viti maalum mkoa wa Tanga Husna Sekiboko kwa kuwapatia simu hizo ambazo zitakwenda kuamsha na kuongeza  ari ya makatibu wa wilaya katika zoezi la usajili ambalo chama hicho limewekeza kuhakikisha tunawapata wanachama wengi zaidi kabla ya uchaguzi wa Serikali za mitaa.

Alisema kuelekea uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyika hivi karibuni wataungana na UWT pamoja na UVCCM ili kuhakikisha  mkoa wa Tanga unashika  namba 1 katika Mikoa yote ya Tanzania bara   kwenye chaguzi zote.

"Hapo awali zoezi la usajili lilikuwa linasua sua ndani ya mwezi huu tumesajili wanachama 735 na kufikisha idadi ya wanachama 9311ambao ni kati ya wanachama 150,000 wa jumuia ya wazazi kwa kupokea vitendea kazi hivi  kutoka kwa mbunge wetu wa viti maalum  tutaendelea kutekeleza jukumu hili la usajili kwa kasi na Ari mpya na lengo letu ni kusajili wanachama 700 ndani ya mwezi mmoja kwa kila wilaya" alisema  

Akizungumza mara baada ya kupokea simu hizo katibu wa umoja wa vijana 'UVCCM' mkoa wa Tanga  amesema Theresia Makiyao amesema mchakato wa usajili wa wanachama wapya kwa upande wao umekuwa ukisuasua  kutokana na uchache wa vitendea kazi lakini kupitia Simu hizo itakuwa ni chachu kwao kuzidi kuongeza wanachama wengi zaidi.

"Ukiangalia kwenye takwimu umoja wa vijana tulikuwa tupo chini sana kwenye usaj mpaka kufikia mwisho wa mwezi Mei  tulikuwa tumesajili wanachama 994 hii ni kutokana na uchache wa vifaa vya usajili lakini  kwa sasa kasi yetu itakwenda juu Sana kwa sababu tayari tumeongezewa nguvu na kasi ya usajili kupitia vifaa hivi ambavyo tumevipoea Leo ila  sisi kama umoja wa vijana tutaingia kazini kwa kampeni maalum kuweza kufanya usajili kwa haraka lengo letu kwa Kila wilaya tumejiwekea  lazima  Kila wilaya iwe imesajili wanachama 500".

Share To:

Post A Comment: