Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa (Mb) amewasili Wilayani Sumbawanga Mkoani Rukwa katika ziara yake ya kikazi na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Charles Makongoro Nyerere leo tarehe 09 Aprili 2024.

Katika ziara hiyo, Waziri Bashungwa atakagua miundombinu ya barabara na madaraja ikiwa ni pamoja na ujenzi wa barabara ya Kaengesa - Chitete, barabara ya Ntendo - Kizungu na upanuzi na ukarabati wa Kiwanja cha Ndege cha Sumbawanga.







Share To:

Post A Comment: