Chama cha Kuweka na Kukopa Cha Lushoto Teachers Saccos Ltd kimetoa mkopo wa Shilingi million 200 kwa wanachama wake Lengo kuwainua kiuchumi.

Akizungumza mara baada ya kikabidhi Hundi, Mwenyekiti wa Bodi ya chama hicho Dk Godwin Maimu alishukuru serikali inayoongozwa na Rais Dk Samia Suluhu Hassan kwa kuweka miongozo ambayo inatoa mwanya wa Taasisi za fedha kutoa mikopo ya riba rafiki kwa Taasisi za wananchi kama SACCOS.

Mbali na kikabidhi Hundi pia walitoa mafunzo maalum juu elimu ya ukopaji yaliyoandaliwa na Chama hicho kwa udhamini wa Benki ya Uchumi na Biashara (UCB) yenye makao yake makuu mkoani Kilimanjaro pamoja na Taasisi iitwayo We Effect yenye makao yake jijini Nairobi Kenya.

Alisema kuwa Chama hicho chenye wanachama zaidi ya 1,000, wengi wao wakiwa Walimu na watumishi wa umma imeleta tofauti kwa kuwawezesha watumishi hao kukopa fedha kwa ajili ya maendeleo yao.




Share To:

Post A Comment: