Kamati ya kudumu ya Bunge  ya uwezeshaji wa mitaji ya umma (PIC)  imetembelea  mradi wa  kuboresha huduma ya maji na usafi wa Mazingira ulioanzishwa na kusimamiwa na Mamlaka ya Maji na usafi wa mazingira AUWSA unaolenga kuondoa changamoto  ya ukosefu wa maji katika Jiji la Arusha na maeneo ya jirani.

Mradi huo ambao umegharimu jumla ya  shilingi Bilioni 520 huku utekelezaji wake ukianza tangu februari 18 mwaka 2016 na kupelekea kupata mafanikio makubwa  ya kutibu maji taka na kuvuna  majisafi yanayo changia  kuongezeka  kwa wingi  wa upatikanaji maji baada ya kukamilika kwakwe  disemba 2023.

Vuma Augustine ni Mbunge wa Kasulu ambaye ndiye Makamu Mwenyekiti wa  kamati ya kudumu ya Bunge ya uwekezaji  ya mitaji ya Umma Vuma ambapo ameeleza kuwa mradi huo utapunguza na kutatua kabisa changamoto  ya ukosefu wa maji kwa wakati katika Jiji la Arusha  na kuwapongeza kwa kukamilisha mradi kwa wakati na uaminifu mkubwa.

Sambamba na hilo Makamu mwenyekiti wa kamati hiyo amewataka AUSWA kuhakikisha wanaendeleza juhudi za kusambaza huduma ya maji kwa wingi katika sehemu mbalimbali  zenye ukosefu wa maji katika Jiji la Arusha kutoka na baadhi ya wananchi kuendelea  kulalamika kukosa huduma ya maji.

 Kama inavyo fahamika jukumu la  AUWSA ni  kusimamia,  kuratibu na kuendeleza Shughuli zote za huduma ya usambazaji wa  majisafi na Huduma za usafi wa Mazingira  katika Jiji la Arusha na maeneo ya pembezoni hivyo  imenzisha utekelezaji wa  mradi huo ili kuendana na kasi  ya  ukuaji wa Jiji hilo.































Share To:

Post A Comment: