Na Imma Msumba ; Arusha 

Rais Samia Hassan Suluhu anatarajia kufungua kikao cha 77 cha Kamisheni ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu kitakachofanyika  Oktoba 20  hadi Novemba 9 ,mwaka huu Jijini Arusha

Akizungumza katika kikao cha Mawaziri cha Kujadili Maandalizi ya Kikao hicho Jijini Arusha Waziri wa Katiba na Sheria,Balozi Dk,Pindi Chana alisema maandalizi  yanakwenda vizuri na  wageni zaidi ya 700 kutoka mataifa mbalimbali watashiriki.

Balozi Chana alisema mbali na kujadili masuala ya msingi yanayohusi haki za binadamu na watu lakini pia  watapata fursa ya  kuitangaza nchi kwa mataifa mbalimbali juu ya utajiri na rasilimali zilizopo nchini.

Alisema kikao hicho kitabainisha mikakati mbalimbali ya  mkutano huo kama fursa ya kiuchumi na kuimarisha taswira ya nchi katika masuala ya haki za binadamu na watu.

Pia taarifa ya hatua iliyofikiwa katika maandalizi ya kikao cha 77 cha kawaida cha kamisheni ya Afrika ya Haki za Binadamu na watu sambamba na kushauri namna bora ya kufanikisha kikao hicho 

"Serikali itatoa ushirikiano katika masuala mbalimbali ikiwemo uwekaji wa mazingira wezeshi katika kufanikisha mkutano huu"

Alisema masuala mbalimbali yatajadiliwa ikiwemo maadhinisho ya siku ya haki za binadamu kwakuzingatia itifaki ya Maputo,taarifa kuhusu hali ya haki za binadamu Barani Afrika,uzinduzi wa nyaraka mbalimbali za kamisheni ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu,taarifa ya wanaharakati wa haki za binadamu na wau,kuidhinishwa kwa itifaki ya mkataba wa Afrika wa Ulinzi wa Jamii.

Lakini pia uwezeshaji wa wanawake katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Hali ya Watu Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi na Ukimwi Barani Afriak na Msaada wa Kisheria na Upatikani wa Haki 

Kwamujibu wa Balozi Chana alisema mkutano huo unahisisha sekta mbalimbali ikiwemo masuala ya kimataifa,utamaduni,sanaa na michezo,fedha na uchumi,ulinzi na usalama ,afya ,habari na mawasiliano.










Share To:

Post A Comment: