NA DENIS CHAMBI, TANGA.
 
UMOJA wa matawi ya wanachama ,  mashabiki na wapenzi kindaki ndaki wa  Klabu ya Simba SC jiji la Tanga wameshiriki kikamilifu kwenye  maadhimisho ya siku ya  timu yao kwa kuchangia damu salama katika Zahanati ya Kisosora ili kuokoa masiaha ya wagojwa wahitaji wa damu wakiwemo  waluopata ajali,  wamama wajawazito na watoto waliopo katika hospital mbalimbali mkoani Tanga .

Akizindua zoezi hilo Mganga mkuu wa mkoa wa Tanga Japhet Simeo amewapongeza mashabiki ,  wapenzi na wanachama wa timu hiyo kwa utayari wao wa  kuona umuhimu wa kuchangia damu ambayo inakwenda kusaidia watu mbalimbali wenye uhitaji akizitaka taasisi,  vikundi na watu binafsi kuendelea kuwa na utamaduni huo ili kuweza kuokoa maisha ya watu wanaofika hospital kupata huduma hiyo.

"Hongereni na nawapongeza na nmefurahi sana kwa mashabiki wa timu ya Simba SC kwa utayari wenu wa kuja kuchangia damu tena kwa hiari yenu,  mimi nawaambia hii ni sadaka na thawabu kubwa sana mliyoitoa kwa wenzenu wenye uhitaji wa damu ,  bado uhitaji wa damu katika hospital zetu ni mkubwa kwa sasa ukilinganisha na wagonjwa ambao wanafika hospitali,  hivyo huu uwe ni mfano wa kuigwa kwa jamii,  wananchi .
,  taasisi na hata mtu binafsi." alisema Simeo.

Mwenyekiti wa matawi ya klabu ya Simba SC Edga Mdime  alisema kama ilivyo ada yao ya kila mwaka bado wanasukumwa kuchangia damu  katika   hospitali wakitambua kuwa uhitaji wa damu ni mkubwa kwa wagonjwa wanaohitaji kuongezewa damu hivyo licha ya kushiriki siku hiyo adhimu kwao bado wanaendelea kuhamasishana kujitoa kwa pamoja katika zoezi hilo.

"Tulianza na zoezi la usafi lakini kubwa zaidi ilikuwa ni kuchangia damu na ni hamasa kubwa sana ambayo imetokea kwa mkoa wetu wa Tanga  kwa wanasimba na matawi yote tumeungana  kwa pamoja kwaajili ya zoezi hili la kuchangia damu"

"Tunajua damu ni muhimu sana kwa kila mmoja wetu,  damu haihusiani na mwana Simba ,  mwana Yanga  au yeyote ila damu ni muhimu sana kwa kila mtu  haswa ukizingatia wapo wakina mama wanaojifungua katika hospitali zetu lakini kuna ajali zinatokea watu wanahitaji kuwekewa damu kwahiyo sisi tunahamasika kama wanajamii ukiachana na swala la michezo" alisema Mdime.

Alisema msimu huu ni wao na lazima makombe yahamie kwao wakijitamba na kikosi kipana ambacho wanacho msimu huu kulingana na usajili mkubwa uliofanyika wakiamini lazima timu hiyo ifanye makubwa katika   mashindano ya ndani na hata kimataifa pia.

Mndime ametuma salamu kwa watani zao timu ya wananchi Yanga  kuelekea mechi za Ngao ya jamii zitakazo chezwa Mkwakwani Tanga ambapo ametamba kwa kusema kuwa hawatakuwa tayari ngao hiyo aichukue tena mtani mbele yao.

"Niwaambie kabisa msimu huu tupo tayari kabisa kunyanyua makwapa hapa hapa Tanga tunaanza na  Ngao ya jamii hiyo lazima tuichukue  kwa usajili ambao tumeufanya hatuna shaka na kikosi chetu msimu huu tupo vizuri sana sana kwa sababu kila nafasi ina mchezaji zaidi ya mmoja tutamfunga Singida na kwenye  fainali yeyote atakayetokea mbele yetu awe Azam au mtani Yanga lazima tutamchapa" alisema Mdime.

Katika dimba la CCM Mkwakwani kuanzia Augost 9 Yanga ambao ni mabingwa watetezi wa Ngao ya jamii watakutana na matajiri wa Chamanzi Azam FC  huku Simba SC wao wakiminyana na Singida Fountain Gate katika hatua ya nusu fainali timu zote zikitafuta nafasi ya kuanza vyema msimu 2023/2024 kwa kuitwaa ngao hiyo.
 
Mkuu wa mabara ya hospital ya rufaa ya mkoa wa Tanga Sinde Ntobu akizungumza na wanachama, mashabiki na wapenzi wa timu ya Simba SC katika Zahanati ya Kisosora mkoani Tanga wakati walipojitokeza kuchangia damu iliyofanyika Augost 5, 2023.
Mwenyekiti wa matawi ya timu ya Simba SC Edga Mndime akipata vipimo kabla ya kwenda kuchangia damu katika Zahanati ya Kisosora.
Mganga Mkuu wa mkoa wa Tanga Japhet Simeo(mwenye koti ) akipewa maelezo na mmoja wa mashabiki wa timu ya Simba baada ya kuzindua zoezi la uchangiaji damu kwenye Zahanati ya Kisosora

Baadhi ya mashabiki wa timu ya Simba SC wakishiriki katika zoezi la uchangiaji damu kwenye zahanat ya Kisosora

 

Share To:

Post A Comment: